Jumamosi, 7 Desemba 2013
Ijumaa, 6 Desemba 2013
Mandela aaga dunia akiwa na umri wa miaka 95
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ametangaza Ijumaa usiku kwamba rais wa zamani mpinzani mkuu wa ubaguzi wa rangi Madiba Nelson Mandela amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu. Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ametangaza Ijumaa usiku kwamba rais wa zamani mpinzani mkuu wa ubaguzi wa rangi Madiba Nelson Mandela amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Akilihutubia taifa Rais Zuma alisema "Taifa letu limempoteza mwana wake mkuu shujaa. watu wetu wamempoteza baba yao"
Mandela alikuwa rais wa Kwanza muafrika kuchukua madaraka kutoka kwa utawala wa ubaguzi wa rangi kutoka kwa wazungu walowachache 1994. Kwa wengi alikua shujaa, mtu shupavu na mwenye mtizamo.
Mara kwa mara alikuwa mnyenyekevu, mchangamfu, muaminifu na mtu ambae aliwajali wananchi wote.
Wasifu wa Mandela
Mwaka 1962, Madiba jina lake maarufu huko Afrika Kusini alikamtwa na kushtakiwa kwa tuhuma za kufanya vitendo vya kutaka kuihujumu serikali. Hata hivyo alijitetea akisema hivyo vilikuwa vitendo vya kuwakomboa waafrika walowengi. Miaka miwili baadae alihukumiwa kifungo cha maisha katika kiswa cha Robben kwenye pwani ya mji wa magharibi wa Cape Town.
Mandela aliachiwa huru miaka 27 badae, ikiwa mwaka 1990 pale serikali ya wazungu wachache iliyokua inaongozwa na Rais Frederik De Klerk kuhalalisha vyama vyote vya kisiasa na kuwafungua wafungwa wote wa kisiasa.
Utawala wa mpito ulienddelea na majadiliano ya kutayarisha katiba na utawala wa kidemokrasia ulianza ukiongozwa na Mandela na De Klerk. Uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vyote na watu wa kabila zote ulifanyika 1994 na Mandela kuchaguliwa akiwa na umri wa miaka 74.
Mandela na mkewe Winnie walikuwa pamoja baada ya kuachiliwa huru kutoka gereza la Robben Island, lakini hai8kuchukua muda wakaachana. Na katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake alipotimiza miaka 80 alimuoa Graca machel, mjane wa rais wa zamani wa Msumbiji Samora Machel.
Alibaki madarakani kwa mhula mmoja wa miaka mitano, na kuanza kampeni chungu nzima moja wapo ikiwa ni kutetea haki za watoto na kupambana na ugonjwa wa Ukimwi. Akiwa madarakani alikosolewa kwa kutokubali kuchukua hatua za nguvu kupambana na janga hilo.
Miaka miwili baada ya kuondoka madarakani mtoto wake wa kiume alifariki kutokana na ukimwi na hapo ndipo aliongeza juhudi zake za kupambana na ugonjwa huo.
Akiwa na umri wa miaka 85 hapo mwaka 1999 Mandela alitangaza kwamba anastahafu kabisa kutoka kazi za umaa lakini aliendelea kufanya kazi kutetea haki za watoto.
Mnamo maisha yake yote alipokea mamia ya tunzo lakini tunzo kuu ni ile ya amani ya Nobel ya 1993aliyopata pamoja na hasimu wake rafiki yake Bw De Klerk.
VOA
Alhamisi, 5 Desemba 2013
Masuala ya Jamii
Ripoti ya Ufaransa: Arafat hakufa kwa sumu
Uchunguzi uliofanywa na wanasayansi wa Ufaransa kuhusu kifo cha kiongozi
wa zamani wa Palestina, Yasser Arafat, umeonyesha kuwa kiongozi huyo
hakufa kutokana na sumu ya Polonium, bali alikufa kifo cha kawaida.
Kwa mujibu wa ripoti ya uchunguzi wa wanasayansi hao, vipimo vimeonyesha
kuwa Arafat alikufa kutokana na uzee baada ya kupata maambukizi na sio
kutokana na sumu ya polonium, ingawa wamesema kulikuwa na ishara za
plotunium.
Matokeo hayo yanatofautiana na ripoti iliyotolewa awali na maabara moja ya Uswisi, iliyoeleza kuwa Arafat alikufa kutokana na kiwango kikubwa cha sumu ya polonium, baada ya kuigundua sumu hiyo kwenye nguo zake.
Ripoti hiyo ya Ufaransa imepingwa vikali na mke wa Arafat, Suha Arafat, ambaye amesema kifo cha mumewe kilikuwa ni mauaji ya kisiasa yaliyofanywa na mtu wake wa karibu. Akizungumza mjini Paris, Suha amesema ameshangazwa na taarifa zinazokinzana kutoka kwa waatalamu wa Ulaya.
Ripoti hiyo iliyokabidhiwa kwa Suha, haitachapishwa, lakini ofisi ya mwendesha mashtaka wa serikali imesema uchunguzi uliokamilika unaoonyesha kuwa Arafat hakuuawa kwa sumu ya polonium.
Arafat, aliyesaini makubaliano ya mjini Oslo ya mwaka 1993 na Israel, alifariki Novemba mwaka 2004 akiwa na umri wa miaka 75, katika hospitali moja nchini Ufaransa.
Kifo chake kilitokea wiki nne alipougua baada ya kula chakula na hivyo kusababisha kutapika na kuumwa tumbo. Taarifa za kitabibu zilionyesha kuwa alikufa kutokana na kutokwa damu katika ubongo, lakini hakukuwa na maelezo ya nini kilisababisha hali hiyo.
Palestina yapuuzia uchunguzi wa Ufaransa
Afisa mwandamizi wa Palestina, Wasel Abu Yousef, ameipuuza ripoti hiyo ya Ufaransa akisema kuwa iko kisiasa zaidi na iko kinyume na ushahidi unaothibitisha kuwa Arafat aliuawa kwa kupewa sumu.
Wapalestina wengi wanaamini kuwa Israel inahusika na kifo cha kiongozi wao, tuhuma ambazo Israel imezikanusha.
Mkuu wa kamati ya Palestina inayochunguza kifo cha Arafat, Tawfik Tirawi amesisitiza kuwa Israel inahusika na awali alisema atataja majina ya watu wanaoaminika kuhusika na kifo cha kiongozi huyo.
Hata hivyo, msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Israel, amesema kuwa ripoti ya matokeo ya Ufaransa si ya kushangaza na kuelezea matumaini yake kwamba sasa Arafat atapumzika kwa amani.
Mwaka uliopita, mjane wa Arafat aliitaka serikali ya Ufaransa ifanye uchunguzi wa kifo cha mumewe, baada ya kituo cha televisheni cha Al Jazeera kuripoti kwamba nguo za Arafat zilikutwa na sumu ya polonium.
Waendesha mashitaka wa Ufaransa walianzisha uchunguzi na hatimaye wataalamu wa kupekuwa ushahidi kutoka Uswisi, Urusi na Ufaransa, walichukua sampuli za mabaki ya mwili wa Arafat, baada ya kufukuliwa mwaka 2012.
Matokeo hayo yanatofautiana na ripoti iliyotolewa awali na maabara moja ya Uswisi, iliyoeleza kuwa Arafat alikufa kutokana na kiwango kikubwa cha sumu ya polonium, baada ya kuigundua sumu hiyo kwenye nguo zake.
Ripoti hiyo ya Ufaransa imepingwa vikali na mke wa Arafat, Suha Arafat, ambaye amesema kifo cha mumewe kilikuwa ni mauaji ya kisiasa yaliyofanywa na mtu wake wa karibu. Akizungumza mjini Paris, Suha amesema ameshangazwa na taarifa zinazokinzana kutoka kwa waatalamu wa Ulaya.
Ripoti hiyo iliyokabidhiwa kwa Suha, haitachapishwa, lakini ofisi ya mwendesha mashtaka wa serikali imesema uchunguzi uliokamilika unaoonyesha kuwa Arafat hakuuawa kwa sumu ya polonium.
Arafat, aliyesaini makubaliano ya mjini Oslo ya mwaka 1993 na Israel, alifariki Novemba mwaka 2004 akiwa na umri wa miaka 75, katika hospitali moja nchini Ufaransa.
Kifo chake kilitokea wiki nne alipougua baada ya kula chakula na hivyo kusababisha kutapika na kuumwa tumbo. Taarifa za kitabibu zilionyesha kuwa alikufa kutokana na kutokwa damu katika ubongo, lakini hakukuwa na maelezo ya nini kilisababisha hali hiyo.
Palestina yapuuzia uchunguzi wa Ufaransa
Afisa mwandamizi wa Palestina, Wasel Abu Yousef, ameipuuza ripoti hiyo ya Ufaransa akisema kuwa iko kisiasa zaidi na iko kinyume na ushahidi unaothibitisha kuwa Arafat aliuawa kwa kupewa sumu.
Wapalestina wengi wanaamini kuwa Israel inahusika na kifo cha kiongozi wao, tuhuma ambazo Israel imezikanusha.
Mkuu wa kamati ya Palestina inayochunguza kifo cha Arafat, Tawfik Tirawi amesisitiza kuwa Israel inahusika na awali alisema atataja majina ya watu wanaoaminika kuhusika na kifo cha kiongozi huyo.
Hata hivyo, msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Israel, amesema kuwa ripoti ya matokeo ya Ufaransa si ya kushangaza na kuelezea matumaini yake kwamba sasa Arafat atapumzika kwa amani.
Mwaka uliopita, mjane wa Arafat aliitaka serikali ya Ufaransa ifanye uchunguzi wa kifo cha mumewe, baada ya kituo cha televisheni cha Al Jazeera kuripoti kwamba nguo za Arafat zilikutwa na sumu ya polonium.
Waendesha mashitaka wa Ufaransa walianzisha uchunguzi na hatimaye wataalamu wa kupekuwa ushahidi kutoka Uswisi, Urusi na Ufaransa, walichukua sampuli za mabaki ya mwili wa Arafat, baada ya kufukuliwa mwaka 2012.
DW.DE
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)