Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2019

Trachoma

Trachoma (Vikope) Trachoma au vikope ni ugonjwa unaosababisha upofu.isitoshe,maabukizi yake yanatokana na bakteria aina ya Klamidia Trakomati. Ugonjwa huu unaweza kuthibitiwa ukitibiwa mapema. Mazingira machafu na ukosefu wa maji safi huchangia maabukizi ya maradhi haya. Nchini kenya jamii za wafungaji wa kuhamahama huadhrikika Zaidi. Hata hivyo idadi ya magonjwa imepungua kwa asilimia 91 kote duniani Kulingana na takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO), idadi ya watu walio kwenye hatari ya maabuziki imepungua kutoka 1.5 billioni mwaka wa 2002 hadi 142 millioni mwaka  2019. Tafiti zinaonyesha kuwa ,kati  ya nchi 44 ambazo ziko Afrika na Asia, zilikubwa na ugonjwa huu lakini umethibitiwa kwa kiwango cha juu kwa sasa. WHO inasema kuwa, idadi ya waliohitaji upasuaji kurekebisha hali ya upofu ya trachoma imepungua kutoka millioni 7.6, mwaka  2002 hadi millioni 2.5 mwaka 2019. Mbali na hayo,serikali ya Kenya imeweka mikakati ya kuto...

ugonjwa wa kifafa

David Kamau ni mkaazi wa Mowlem viungani vya jiji la Nairobi. Toka utotoni yeye anaishi na ugonjwa wa kifafa.Kwa muda mrefu,wazazi wake walitafuta tiba za kienyeji kwa waganga wa kienyeji bila mafanikio. Walisema mtoto wao amefanyiwa uchawi ila hawakufahamu kuwa aliugua kifafa. Mara kwa mara Kamau alipoteza fahamu na kuzimia,alianguka na akapoteza muda mwingi kutafuta tiba.Hakuendelea na masomo yake baaada ya kidato cha nne. Kamau ni miongoni mwa watu robo tatu walio na ugonjwa wa kifafa katika nchi zenye kipato cha chini , na ambao hawapati matibabu wanayoyahitaji. Hii inachangia kuwepo hatari ya kufa kabla ya wakati wao. Kulingana na   ripoti mpya ya shirika la afya duniani WHO baadhi ya wagonjwa wa kifafa hawapati matibabu inavyostahili. Zaidi ya hayo wengine wanaogopa kwenda hospitalini kwa sababu ya unyanyapa,na pia Imani potovu zinazohuzishwa na ugonjwa huu. WHO inasema endapo wagonjwa wangepata matibabu na kwa haraka hali yao ya kiafya ingekuwa ...

WHO in Uganda

Picha
Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Dr. Tedros Adhanom Ghebreyesus,azuru Uganda kutadhimini hali ilivyo kwa sasa,baada ya mripuko wa Ebola huko Kasese, Uganda. WHO photo Dkt Ghebreyesus aliwasiri Uganda kutoka Congo ambapo alitembelea maeneo ya mkurupuko wa Ebola,huko Butembo na Katwa. Kwenye taarifa, Mkurugenzi mkuu alitoa hakikisho kuwa shirika lake litajitahidi kuhakikisha kuwa ugonjwa wa Ebola umekabiliwa. Alisema hali sio nzuri, hadi ugonjwa wa Ebola ukabiliwe Congo. Hata hivyo alisema kuna mafanikio ya kupungua kwa maradhi hayo hasa Butembo na katwa. Isitoshe, kwenye kikao katika nchi hizo mbili,alitilia mkaso kuwa endapo idadi ya maabukizi ya Ebola yamepungua, si vema kuweka Imani kuwa hali iko sawa. Aliongeza kuwa ni muhimu kwa wadau wa afya na serikali kulichukualia kwa uzito tishio hili ili kuepuka milipuko Zaidi. Alisema sehemu ya Mabalako ambapo ugonjwa huu ulipolipuka mara ya kwanza   mwaka wa 2018,imekuwa ni sehemu ambapo mi...

world blood donor day 2019

Picha
Kesho ( June 14, 2019) ni siku ya maadhimisho ya utoaji damu duniani. Siku hii   ambayo huadhimishwa kila mwaka,imelenga kuwashukuru watu wote wanaojitokeza kutoa damu kwa hiari ili kuokoa maisha ya wagonjwa waliopungukiwa na damu na pia   walio kwenye   hatari ya kupoteza maisha kwa kukosa damu.   Shirika la Afya duniani (WHO) na nchini wanachama wake zimelenga   kuwaelimisha watu    umuhimu wa kujitolea kutoa   damu mara kwa mara ili kuongeza paini za damu safi na salama kote duniani Nchini Kenya kumekuwa na upungufu wa damu katika kituo cha Kitaifa cha kuhifadhi damu maana wakenya wengi hawapendi kutoa damu. Mila,tamaduni na pia Imani za kidini zikichangia katika hali hii. Serikali imekuwa katika harakati za kuwahamazisha wakenya umuhimu wa kutoa damu ilikuokoa maisha ya maelfu ya watu wanaokumbana na matatizo ya ukosefu wa damu ya kutosha mwilini. Maadhimisho haya yatafanyika nchini Rwanda, maudhui yakiwa “damu sala...

Ebola death Uganda

Picha
Kenya imechukua hatua za dharula kuthibiti ugonjwa wa ebola baada ya kijana mmoja kufariki huko Kasese ,Magharibi mwa Uganda .  Wizara ya Afya imesema kuwa wataalamu wa afya wamepelekwa   kwenye  vituo vya mipaka yake kuthibitisha virusi vya Ebola. Doria imewekwa  mipakani  hasa katika viingilio vyaa Busia ,Malaba na pia kwenye Viwanja vya ndege. Kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya Kenya, wageni  wanaoingia kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Uganda,Rwanda ,Burundi  na nchi nyingine wanafanyiwa uchunguzi na watalamu wa afya ,kabla kuruhusiwa kuingia nchini. Watapimwa viwango vya joto mwilini. Katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta, Chumba maalum cha uchunguzi kimetengwa ili kukabiliana na maradhi haya endapo yatagunduliwa .Pia kuna Sehemu maalum ya matibabu (Vituo vya udhibiti)katika hospitali kuu ya Kenyatta. Uganda ilitangaza kesi mbili za Ebola baada ya kugunduliwa kwa kijana mwenye umri wa mia...

The WHO Academy Lyon hub

Picha
(WHO photo) Shirika la afya duniani likishirikiana na serikali ya Ufarasa imeweka mkataba wa pamoja kushirikiana katika harakati zake za kuanzisha chuo cha mafunzo ya afya duniani huko Lyon,Ufaransa. Makubaliano hayo yalifanywa na Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom Gebreyesus na   Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron huko Geneva,Uswizi. Chuo hicho kinatarajiwa kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya na kiafya na wadau wake  duniani kote. WHO Academy Lyon Hub kama kitakavyojulikana,kitakuwa ni chuo cha hali ya juu yenye mafunzo na teknologia ya kisasa. Wabunifu watapata fursa kuonyesha ubunifu wao na kuchangia katika mundo mbinu ya afya,katika harakati za kuinua viwango na huduma za afya duniani. Kulingana na Shirika la Afya Duniani(WHO)lengo la kufanya maazimiyo hayo na    nia ya kuanzisha chuo cha mafunzo ya afya ni kufanikisha shabaha ya WHO la kuhakikisha kuwa ifikiapo mwaka wa 2023 watu billioni moja watafaidika kutokana na huduma bora za ...