Ijumaa, 7 Juni 2019

FAO chakula salama



Chakula salama ni jukumu la kila mmoja

Leo ni siku ya usalama wa chakula duniani.


Huku siku hii ikiadhimishwa kote duniani ni jukumu ya kila mmoja kuhakikisha chakula anakinunua na kula ni salama kwa matumizi.


Mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani (WHO)Dkt Tedros Adhanon Ghebreyesus anasema hii ni fursa muhimu kuhamasisha juu ya hatari za chakula kisicho salama kwa wote hususan serikali,wazalishaji na watumiaji .
Image result for SOKO YA MBOGA NA MATUNDA
Anasizitisha kuwa sisi sote tuna jukumu ya kuhakikisha chakula ni salama kutoka shambani hadi kwenye sahani.

Hivi karibuni kumekuwa na taarifa kuwa chakula kinacholiwa nchini Kenya kina kemikali ambazo husababisha maradhi kwa watu.

Tafiti zinaonyesha kuwa mboga aina ya sukumawiki ina madini yenye sumu na ni hatari kwa maisha ya mwanadamu.

Wakenya hasa wanaoishi jijini Nairobi na viunga vyake wamo hatari kwani imebainika mboga wanazonunua zina madini kama vile zebaki,shaba na chama.
Image result for sukumawiki

Zina viwango za juu Zaidi ya ilivyohalalishwa na shirika la afya duniani.

Chakula aina ya mboga zinazotumiwa sana Nairobi ni kama vile;nyanya,vitungu,kabeji na karoti.
Kwa mfano kilo moja ya mboga hizo ilifanyiwa utafiti katika maabara za KEPHIS na ile ya kibinafsi ya ANALAB .Matokeo ya sampuli kutoka maduka inaonyesha zilikuwa na 0.13mg kwa kila kilo na 0.15 kwa kila kilo ya zebaki, ambayo ni Zaidi ya viwango vilivyo ratibiwa na kuidhinishwa na shirika la afya duniani vya 0.1 kwa kila kilo.


Ripoti pia inaonyesha kuwa mboga kutoka masoko ya korogocho ilirekodi kiwango cha juu cha zebaki cha 0.11 .Imedainika kuwa kila mwaka watu zaidi ya milioni 600 huadhilika kwa kula vyakula vilivyo na chemikali na madini yenye sumu huku wengine 42,000 wakifariki kila mwaka.

Hali hii pia uchangia pakubwa kuzorota kwa uchumi ,biashara na sekta ya utalii

Zaidi ya hayo,takwimu za Mashirika ya  umoja wa mataifa yanayohusika na afya,chakula na kilimo zinakadilia takribani dola bilioni 95 zinazopotea kila mwaka kutokana na chakula kisichofaa kwa nchi zinazoendela .

Ni jukumu la mataifa kuhakikisha chakula kimelindwa .
Pia ni wajibu wakila mmoja kuchukua hatua muafata kuona kua usalama wa chakula umedumishwa.


Wanaukuza chakula ,wauzaji na wanaokula hicho chakula wana majukumu yakulinda chakula,kwani chakula kisafi,afya njema.


Madini haya hupatikana kwenye maji yanyotoka viwandani vya magari,rangi na wakati yanatumiwa maji hayo husababisha mimea kuwa na viwago vya juu vya madini  na kemikali zenye sumu.


Hatua madhubuti zichukuliwe kuhakikisha chakula kimedhibitiwe na serikali kuhakikisha ni salama.


Tekinologia ya kisasa ya kudhibiti chakula ili kuhakikisha ni salama ;inahitajika.

Serikali pia zinamajukumu ya kuwaelimisha wananchi jinsi ya kutunza mazingira ili kuepukana na hatari za chakula chenye sumu.

Ni muhimu kujiepusha kununua vyakula vya mitandao ambayo asili yake si hakika.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni