Maambukizi ya magonjwa ya zinaa ya
ongezeka
Magonjwa ya zinaa yaongezeka, huku takwimu
zikionyesha kuwa kuna maambukizi ya Zaidi ya millioni moja kila siku.
Kwa mujibu wa Shirika la afya ulimwenguni, WHO.
Waadhiriwa wa maradhi ya zinaa ni watu wa umri wa miaka 15 hadi 49.
Magonjwa hayo ni kama vile,kisonono,kaswende ,trichomoniasis na klamidia
Magonjwa haya yanaadhari katika
maisha ya anayeugua.
Kukosa au kupoteza ujauzito, watoto
kufia tumboni kwa akina mama na pia hatari ipo kuambukuzwa HIV.
Wataalamu wa afya wa WHO wnadokeza
kuwa mtu mmoja kati ya 25 duniani kote ana aina moja ya maradhi ya zinaa.
Huku wengine wakiwa na maabukizi ya magonjwa
Zaidi kwa wakati mmoja.
Takwimu za mwisho kuchapishwa na WHO
mwaka wa 2012 zinaashiria kuwa maambukizi ya magonjwa ya zinaa yanazidi
kuongezeka kila uchao.
Zaidi ya hayo,wito umetolewa kwa kina
mama wajawazito kufanyiwa uchunguzi wa mara kwa mara hasa kwa maradhi ya
kaswende na HIV ili kupunuza vifo zaidi
Hata kama inaaminika magonjwa haya yana tiba,
changamoto iiliyopo kwa sasa ni upungufu wa dawa aina za benzathine penicillin
zinazotibu hasa kaswende.
Dalili
Dalili hutofautiana
baina ya wnawake na wanaume.
Wanaume huona
dalili za maradhi ya zinaa siku chache baada ya kushiriki ngono huku akina mama
hukukua muda mrefu; wiki au miezi baada ya kuambukizwa.
- · Kutoka usaha kwenye njia ya haja ndogo
- · Kusikia maumivu wakati wa kujisaidia haja ndogo
- · Kutokwa na uvimbe au vidonda sehemu ya uke au ya ume
- · Kutokuwa na hamu ya kushiriki ngono.
- · Kuvuja damu kabla ya muda wa hedhi
Matumizi ya
mipira ya kondom wakati wakushiriki ngono yanapendekezwa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni