Jumatatu, 17 Juni 2019

WHO in Uganda


Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Dr. Tedros Adhanom Ghebreyesus,azuru Uganda kutadhimini hali ilivyo kwa sasa,baada ya mripuko wa Ebola huko Kasese, Uganda.

Who 703x422
WHO photo
Dkt Ghebreyesus aliwasiri Uganda kutoka Congo ambapo alitembelea maeneo ya mkurupuko wa Ebola,huko Butembo na Katwa.
Kwenye taarifa, Mkurugenzi mkuu alitoa hakikisho kuwa shirika lake litajitahidi kuhakikisha kuwa ugonjwa wa Ebola umekabiliwa.

Alisema hali sio nzuri, hadi ugonjwa wa Ebola ukabiliwe Congo.

Hata hivyo alisema kuna mafanikio ya kupungua kwa maradhi hayo hasa Butembo na katwa.

Isitoshe, kwenye kikao katika nchi hizo mbili,alitilia mkaso kuwa endapo idadi ya maabukizi ya Ebola yamepungua, si vema kuweka Imani kuwa hali iko sawa.

Dr Tedros holds discussion with Prof Omaswa and WHO Representative in Uganda Dr Yonas Aliongeza kuwa ni muhimu kwa wadau wa afya na serikali kulichukualia kwa uzito tishio hili ili kuepuka milipuko Zaidi.

Alisema sehemu ya Mabalako ambapo ugonjwa huu ulipolipuka mara ya kwanza  mwaka wa 2018,imekuwa ni sehemu ambapo milipuko Zaidi imeripotiwa.

Hii pia ni sehemu watu waliopatikana na Ebola Uganda walitokea.

Nchi za Uganda na Kenya zimeweka tahadhari mipakani tangu kuzuka kwa ebola na kifo cha kijana mmoja aliyetokea huku Jamhuri ya Demokrasia ya Congo wiki moja iliyopita.
Photo PPU


Baadaye Dkt Ghebreyesus,akiadamana naWaziri wa Afya na maafisa wa afya alikutana na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Mseveni kuhusu tishio la Ebola Uganda.
Alipongeza Uganda kwa hatua walizochukua kufuatia mlipuko wa ebola hivi majuzi.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni