Jumanne, 4 Februari 2020


Rais Mstaafu Daniel T Moi Aaga Dunia
Moi: The herdsboy who became Kenya's second president
Rais  mstaafu Daniel  Arap Moi ameaga dunia .


Mzee Moi  ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 95 katika hospitali ya Nairobi alipokuwa amelazwa tangu mwezi wa kumi mwaka jana.

Kundi la madaktari likiongozwa na Daktari wake wa miaka mingi, David Silverstein limekuwa likimpa mkatibabu kwa matatizo yanayojirejeeza na kumfanya kusalia kitandani kwa miezi mitatu.

Hali ya afya ya mzee Moi ilidorola Mwezi uliopita huku  madaktari wake  wakilazimika kumrejesha Moi katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Kifo chake alfajiri ya leo kimetangazwa na Rais uhuru Kenyatta ambaye ni mwanafunzi na mwanawe wa kisiasaAwali,msemaji wake Lee Njiru  alisema Moi alikuwa amekwenda hospitali kwa ukaguzi wa kawaida wa afya lakini tangu wakati huo,amekuwa ndani nan je ya hospitali.
Mzee Moi, alijeruhiwa kwenye  goti alipohusika kwa ajari  iliyohusisha gari lake mwaka wa 2006 huko Limuru .


Moi alichukua hatamu za uongozi mwaka wa 1978,baada ya kifo cha Mwanzilishi waTaifa Marehemu Rais Jomo Kenyatta.


Kama mwandishi wa maswala ya afya nitamkubuka Rais Moi kama kiongozi aliyejari afya na malezi bora kwa watu hasa  watoto .Alihakikisha watoto walipata maziwa ya bure shuleni.


Pia alitilia mkazo mpango wa uzazi kwa akina na mama kwa minajiri ya afya bora na malezi mema.

Pia alijulikana kwa kuwa mtu aliyejali afya yake kwa kula vyakula vyene afya mwilini.

Kuhusu mazingira,Moi aliweka sera kuhakikisha wakulima wamepata miti ilikuzuia momonyoko wa udongo.


Alikuwa kwenye mstari wa mbele pia katika maswala la dini.

Rais alikuwa mkarimu, alipozuru sehemu tofauti za nchi aliwatunuku akina mama na watoto waliojitokeza kumlaki.

Pia alikuwa mcha Mungu.Kila jumapili rais hangekosa kanisani.


Mola ailaze roho ya Marehemu Rais Daniel Toritich Arap Moi palipo watakatifu wake.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni