Malaria Kenya
Idadi ya wagonjwa wa malaria yapungua Kenya Ugonjwa wa malaria umekuwa ni tisho katika maeneo yenye joto Afrika hususan nchini Kenya. Jambo la kutia moyo ni kwamba iadadi ya watu wanaougua ugonjwa huu umepungua marudufu kwa miaka sita iliyopita. Kulingana na tafiti za wizara ya Afya hali hii inatokana na ongezeko la utumiaji viandarua na pia kupata matibabu mapema.Msemaji wa wizara ya afya Elisha Omondi anasema hatua za serikali za kuukabili ugonjwa wa malaria zimezaa matunda. Hata hivyo sehemu kama vile jimbo la Siaya linaongoza kwa maambukizi hayo,lakini pia katika kipindi cha mwaka mmoja angalau asilimia 50 ya visa vimekabiliwa. Majimbo ya Pwani pia yameadhirika lakini hali sio mbaya kama siku za nyuma. Takwimu sinaonyesha kuwa Malaria iliwaua karibu watu nusu milioni duniani mwaka jana, huku vifo tisa juu ya kumi vikitoka kusini mwa Sahara. Kenya ni miongoni mwa mataifa ya kusini mwa Jangwa la Afrika ambapo Malaria imeandelea kuangamiza watu lak...