Idadi ya wagonjwa wa malaria yapungua Kenya
Ugonjwa wa malaria umekuwa ni tisho katika
maeneo yenye joto Afrika hususan nchini Kenya.
Kulingana na tafiti za wizara ya Afya hali hii inatokana na ongezeko la utumiaji viandarua na pia kupata matibabu mapema.Msemaji wa wizara ya afya Elisha Omondi anasema hatua za serikali za kuukabili ugonjwa wa malaria zimezaa matunda.
Hata hivyo sehemu kama vile jimbo la Siaya linaongoza kwa maambukizi
hayo,lakini pia katika kipindi cha mwaka mmoja angalau asilimia 50 ya visa
vimekabiliwa.
Majimbo ya Pwani pia yameadhirika lakini hali
sio mbaya kama siku za nyuma.
Takwimu sinaonyesha kuwa Malaria iliwaua karibu watu nusu milioni
duniani mwaka jana, huku vifo tisa juu ya kumi vikitoka kusini mwa Sahara.
Kenya ni miongoni mwa mataifa ya kusini mwa Jangwa la Afrika ambapo
Malaria imeandelea kuangamiza watu lakini hali hii imeimarika kwa asili mia nane ikilinganishwa na hali
ilivyokua miaka sita iliyopita.
Isistoshe, wanawake waja wazito na watoto wako hatarini zaidi na
wanatakikana wanapokea matibabu punde
zinapojitokeza dalili za ugonjwa kwani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni