Uchina umekuwa kitovu cha virusi, na
kufikia sasa watu 81,291wameambukizwa vurisi hivi ulimwenguni kote na kuwauwa
2,770, wengi wao wakiwa katika taifa la Asia.
Serikali kwa upande wake imesema hakuna
haja ya kuhofia maambukizi kwani mikakati dhabiti imewekwa kuhakikisha hakuna
mtu atakayeingia nchini bila kukaguliwa au kuchunguzwa iwapo ana virusi au la.
“Hatua zote za tahadhari zimewekwa na kila
mtu anayekuja nchini hupimwa vya ipasavyo na watalamu wa afya.
Awali serikali ilisema kuwa mipaka na
viwanja vya
ndege na pia bandarini hali imedhibitiwa.
Hata hivyo wakenya hawajaridhishwa na hatua
ya serikali ya kutowarejesha wakenya 91 waliokwama nchini uchina.
Familia za wahusika sinasema kuwa wapendwa
wao wamo hatarini yakuambukizwa virusi na pia kuadhirika kimawazo maana
hawatoki nje na pia kuna upungufu wa chakula.
Kufikia sasa visa 15 vimefanyiwa tafiti
kwenye mahabara kuhakikisha kuwa watu wote walioonyesha dalili za Corona wako
salama.
·
Pia
Mipango ya kuhamasisha umma kuhusu jinsi ya kukambiliana na virusi vya Corona
endapo vitaripotiwa imewekwa.
·
Kitengo
cha dharura chenye maafisa wenye majukumu ya kufatilia na kuchunguza kisa
chochote kinachorioptiwa nchini
·
Vifaa vya
kutosha kuwekwa kwenye vituo maalum vya kuchunguza virusi kwa wasafiri wote
wanaoingia nchini kutoka mataifa mbalimbali.
·
Mafunzo kwa
maafisa wa afya huku maafisa mia tano wakifunzwa katika vituo vya afya vya umma
na pia vya kibinafsi.
·
Wananchi
wameshauriwa kuwashiriana na Wizara ya Afya kuripoti kisa chochote
kinachshukiwa kuwa cha Corona.
Shirika la Afya Duniani lasema dunia sharti
ijiandae kukambili na janga la virusi vya Corona
Mkuu wa WHO
Tedros Adhanom Ghebreyesus anasema Virusi vya Corona vinaweza kuwa janga
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni