David Kamau ni mkaazi wa Mowlem viungani vya jiji la Nairobi.
Toka
utotoni yeye anaishi na ugonjwa wa kifafa.Kwa muda mrefu,wazazi wake walitafuta
tiba za kienyeji kwa waganga wa kienyeji bila mafanikio.
Walisema mtoto wao amefanyiwa uchawi ila hawakufahamu kuwa aliugua
kifafa.
Mara kwa mara Kamau alipoteza fahamu na kuzimia,alianguka na
akapoteza muda mwingi kutafuta tiba.Hakuendelea na masomo yake baaada ya kidato
cha nne.
Zaidi
ya hayo wengine wanaogopa kwenda hospitalini kwa sababu ya unyanyapa,na pia Imani
potovu zinazohuzishwa na ugonjwa huu.
WHO
inasema endapo wagonjwa wangepata matibabu na kwa haraka hali yao ya kiafya ingekuwa
bora.
WHO
inasema pengo la ukosefu wa matibabu au huduma za afya karibu na waathiriwa
linaweza kizibwa .Asili mia 70 wana kifafa.
Inasema
kuwa hali si sawa katika mataifa yenye chumi ndogo ikilinganishwa na mataifa yaliyostawi
kiuchumi.Vifo vya mapema ni Zaidi katika nchi zenye chumi ndogo.Watu wenye
kifafa wanakunwa na magonjwa mengine ya kiakili na hii inashababisha kuzorota kwa
hali ya mtu.
WHO
inakadiria kuwa kuna wa millioni mia tano (500) wenye kifafa kote duniani.
Nchini
kenya hali sio tofauti .Watu millioni moja wana kifafa huku wawili kati ya mia
hawajapata tiba au hawafahamu kuwa wana hali hii.
Watu millioni 2.4 hupatikana na kifafa duniani
kote kila mwaka.
Vifo
hutokea hasa wakati mtu anapozama maji,majeruhi ya kichwa au kuchomeka mtu
anapopata mshtuko.
Jinsi ya kumsaidia mtu anapopata mshtuko wa kifafa.
Jinsi ya kumsaidia mtu anapopata mshtuko wa kifafa.
- Unastahili kushikilia kichwa cha mgonjwa
- Kichwa kinapaswa kugeuswa kwa upande
- Usijaribu kufungua kinywa au kuweka kijiti au kijiko
- Endapo shambulio litapita dakika tano,unapaswa kutafuta ambulensi kwa dharula.
- Asipewe chakula wala maji
- Shambulio hudumu dakika 2-3 kwa kawaida.
- Usimuamushe hadi apate fahamu
Hali ikizidi tafuta usaidizi wa mtaalam wa afya.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni