Alhamisi, 6 Juni 2019

FGM women deliver



Ukeketaji ni kuondoa sehemu ya nje ya uke na katika tamaduni na mila za jamii zingine ni kuondoa sehemu yote na kuishona.

Lakini Kenya imepiga hatua marudufu kukabiliana na tishio hili ambalo limepitwa na wakati
Ni kufuatia hatua hii Rais wa Kenya ,Uhuru Kenyatta akiongea katika kongamano la usawa wa jinsia inayoendele nchini Canada Rais wa kenya uhuru Kenyatta amesema Kenyaiko katika mstari wa mbele kutokomesha upasaji tohara.
Image result for uhuru kenyatta women deliver 2019 picsRais Kenyatta alisema imepiga hatua kuhakikisha tishio la ukeketaji limekabiliwa ifikapo mwaka wa 2022
Mikakati pia imechukuliwa kuhakikisha ndoa za mapema zimekomeshwa huku masomo ya shule ya upili yakiwa ni lazima kwa kila mtoto kuhudhuria.
Alisema hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mzazi au mtu yeyote atakaye zuia au kumkataza mtoto haki yake ya masomo.
Swala la ukeketaji limekua changamoto hapa nchini Kenya na Bara la Afrika kwa jumla.
Mila ya ukeketaji imekidhiri katika sehemu tofautia nchini Kenya.Hata baada ya kupigwa marufuku,wengi ufanya tendo hili ,japo kwa usiri.

Figure
Majimbo ya Migori,Meru,Taita taveta,Kisii ,Narok,Kajiado na pia Kaskasini Mashariki na Pwani yakiadhirika Zaidi.

Ukeketaji hutofautiana na tamaduni na mila  za kabila lakini lengo ni kuhakikisha au kulinda mwanamke katika matamanio yake ya kujamiiana.

Tishio hili limesababisha akina mama kuwa hatarini hasa wakati wanapojifungua;wanapata matatizo ya kisaikolojia.

Image result for fgm
Hata hivyo,katika sehemu  ukeketaji umeshamili,unyanyapaa kwa wale sio keketwa unatisha.
Wanawake huchekwa na walio kwenye ndoa hudharauliwa na kukejeriwa na wanawake wenzao waliokeketwa.

Kumekuwa na matukio ambapo akina mama walioolewa kulazimishwa kukeketwa .Mara kwa mara wao hufumaniwa wanapotuka katika shughuli zao za kila siku.

 Kulingana na takwimu za shirika la afya Duniani WHO,wasichana na akina mama Zaidi ya millioni 200 wamekeketwa huku wengine millioni 3 wakiwa kwenye hatari za kukeketwa.Wao wako kwa  umri wa miaka 15 hadi 49.

Zaidi ya hayo,bara la Asia,mataifa ya uarabuni pia simetajwa kama bara zinazoendeleza mbinu hii potovu kwa juu sana.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni