Dawa ya kupanga uzazi kwa wanaume
kufanyiwa majaribio katika hospitali kuu ya Kenyatta nchini Kenya.
Kulingana na mila na tamaduni za kiafrika
kupanga uzazi ni mwiko.
Hata hivyo desturi na tamaduni hizi
zimepitwa na wakati;ijapo kukuwa wachache wamezifuatilia na kuziheshimu.
Zaidi ya hayo maswala ya upangaji uzazi
kwa wanaume yanazungumziwa kwa siri sana.
Kasuba ilioko ni kuwa uzazi mpango ni
majukumu ya akina mama.
Wao hupata maradhi yanayotokana na
mayumizi ya aina mbalimbali za mpango uzazi.
Hivyo basi watafiti na wataalam wa afya
wamebuni mbinu mpya ya kuhakikisha kuwa swala la uzazi mpango ni jukumu la kina
mama pekee.Wanaume pia wapaswa kujumuishwa kwenye shughuli hii muhimu.
Ni kufuatia tafiti hii,hospitali ya
Kenyatta na chuo kikuu kimoja kutoka Marekani imezidua utafiti wa dawa ya
kupanga uzazi kwa wanaume.
Dawa hii itatumiwa kupaka katika sehemu
ya kusoto ya mbega kwa muda wa wiki 40.
Pia mbegu za kiume zitachukuliwa kufajiwa
uchunguzi wa kiafya.Huku jaribio hili likitarajiwa kuchukua wiki 4(nne) hadi 8
(nane).
Mpango huu unatumainiwa kuchukua muda wa
miaka miwili kupata mapokeo mwafaka.
Watakaoshiriki kwenye utafiti huu ni watu
walio kwenye ndoa itakayodumu kwa muda mrefu.
Hata hivyo mwanamke ataendelea kupanga
uzazi hadi muda uliotengwa kufanya uchunguzi kwa mwanaume kuisha.
Mwanaume anayetarajia kufanya uzazi
mpango sharti awe na umri wa kati ya miaka 18 hadi 50 huku mwanamke akiwa na
umri wa 14 hadi 34.
Aina tofauti za uzazi wa mpango.
·
Kuweka Kitanzi
·
Kuweka kipandikizi/ Kijiti
·
Njia ya Vidonge
·
Njia ya sindano
·
Kutumia mipira ya kondom ya kike au ya kiume
Aina hizi huwa na
madhara kwa akina mama kama vile;
Kupata ugumu wa
kushika mimba baadaya ya matumizi ya muda mrefu,kuvunja damu mara kwa
mara,kupungua au kuongezea kwa mwili na mabadiliko ya siku za hedhi.
Endapo
ufanisi utapatikana kwenye jaribio hili basi itapunguza changamoto zinazowakabili
wanawake katika shughuli zao za kuhakikisha wamepanga uzazi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni