Kesho
(June 14, 2019) ni siku ya maadhimisho
ya utoaji damu duniani.
Siku hii ambayo huadhimishwa kila mwaka,imelenga kuwashukuru watu wote wanaojitokeza kutoa damu kwa hiari ili kuokoa maisha ya wagonjwa waliopungukiwa na damu na pia walio kwenye hatari ya kupoteza maisha kwa kukosa damu.
Nchini Kenya kumekuwa na upungufu wa damu katika kituo
cha Kitaifa cha kuhifadhi damu maana wakenya wengi hawapendi kutoa damu.
Mila,tamaduni na pia Imani za kidini zikichangia
katika hali hii.
Serikali imekuwa katika harakati za kuwahamazisha
wakenya umuhimu wa kutoa damu ilikuokoa maisha ya maelfu ya watu wanaokumbana
na matatizo ya ukosefu wa damu ya kutosha mwilini.
Maadhimisho haya yatafanyika nchini Rwanda, maudhui
yakiwa “damu salama kwa wote (safe blood for all).
Utoaji
wa damu unasaidia kuokoa maisha ya mamilioni ya watu kila mwaka kwani wagonjwa
wanaougua na kuhatarisha maisha huokolewa na damu ambayo iko katika hifadhi au
benki ya damu.
Wagonjwa
wa dharula, wanaofanyiwa upasuaji wakiwemo wamama wanaotoka kujifungua ni
miongoni mwa wale wanaonufaika na damu iliotolewa na watu kwa hiari.
Nchi
nyingi zinakumbana na tatizo la upungufu wa damu katika benki za damu na tatizo
la kupata damu safi na salama .
Ni
jambo la muhimu watu kuelimishwa na kutambua mafanikio yanayotokana na kuchanga
damu safi na salama.
Hatua
hii itasaidia watu wengine walioko hospitalini wanaoteseka na tatizo la
upungufu wa damu mwilini.
Shirika
la kuhifadhi damu nchini Kenya (KNBTS),) inasema kuwa Kenya haijafikia viwango vya paini za damu
iliyowekewa na shirika la Afya Duniani,kwa nchi wanachama
wake.
Kulingana
na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), nchi inapaswa kuwa na paini 400,000 za
damu kila wakati.
Hata hivyo,kiwango hiki kinaweza kufikiwa iwapo asilimia moja ya
watu wangetoa damu mara moja kwa mwaka
sababu ikiwa watu wengi
hawapendi kutoa damu na pia watu kukosa
kuelewa umuhimu wa kutoa damu.
Kwa muda mrefu KNBTS imekuwa ikihamasisha Wakenya kujitokeza
kutoa damu kupitia mitandao ya kijamii vyombo vya habari na mabango.
ajari za barabarani, mashambulizi ya kigaidi na kuongezeka kwa
magonjwa yanayohitaji damu Zaidi yamechangia upungufu wa damu katika hifadhi.
Utoaji wa damu Kenya uko chini sana huku idadi ya wanaohitaji
damu ikiongezeka kila siku.
Itakuwa changamoto kwa wakenya nan a watu wote kujitolea kutoa
damu ili kuokoa maisha ya marafiki,wapendwa wetu n ahata watu tusiowafahamu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni