Jumatano, 12 Juni 2019

The WHO Academy Lyon hub



Image result for who LOGO
(WHO photo)
Shirika la afya duniani likishirikiana na serikali ya Ufarasa imeweka mkataba wa pamoja kushirikiana katika harakati zake za kuanzisha chuo cha mafunzo ya afya duniani huko Lyon,Ufaransa.

Makubaliano hayo yalifanywa na Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom Gebreyesus na  Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron huko Geneva,Uswizi.

Chuo hicho kinatarajiwa kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya na kiafya na wadau wake  duniani kote.

WHO Academy Lyon Hub kama kitakavyojulikana,kitakuwa ni chuo cha hali ya juu yenye mafunzo na teknologia ya kisasa.

Wabunifu watapata fursa kuonyesha ubunifu wao na kuchangia katika mundo mbinu ya afya,katika harakati za kuinua viwango na huduma za afya duniani.

Kulingana na Shirika la Afya Duniani(WHO)lengo la kufanya maazimiyo hayo na  nia ya kuanzisha chuo cha mafunzo ya afya ni kufanikisha shabaha ya WHO la kuhakikisha kuwa ifikiapo mwaka wa 2023 watu billioni moja watafaidika kutokana na huduma bora za afya kote duniani.

Mafunzo yatatolewa na wataalamu wa afya kulingana na kanuni na malengo ya shirika la afya duniani(WHO).

Viongozi,wasomi,watafiti ,wafanyi kazi wa WHO, watu wote duniani waliohitimu watapewa nafasi ya masomo katika chuo hiki.Ni sharti watoke nchi wanachama wa WHO.

Shirika la Afya Duniani(WHO) limekuwa kwenye mstali wa mbele kuhakikisha wato kote duniani wamepata huduma bora ya afya .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni