Alhamisi, 13 Juni 2019

Ebola death Uganda



Kenya imechukua hatua za dharula kuthibiti ugonjwa wa ebola baada ya kijana mmoja kufariki huko Kasese ,Magharibi mwa Uganda . 

Wizara ya Afya imesema kuwa wataalamu wa afya wamepelekwa   kwenye  vituo vya mipaka yake kuthibitisha virusi vya Ebola.

Doria imewekwa  mipakani  hasa katika viingilio vyaa Busia ,Malaba na pia kwenye Viwanja vya ndege.

Image result for kenya boader surveillance ebola
Kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya Kenya, wageni  wanaoingia kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Uganda,Rwanda ,Burundi  na nchi nyingine wanafanyiwa uchunguzi na watalamu wa afya ,kabla kuruhusiwa kuingia nchini.
Watapimwa viwango vya joto mwilini.
Katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta, Chumba maalum cha uchunguzi kimetengwa ili kukabiliana na maradhi haya endapo yatagunduliwa .Pia kuna Sehemu maalum ya matibabu (Vituo vya udhibiti)katika hospitali kuu ya Kenyatta.

Uganda ilitangaza kesi mbili za Ebola baada ya kugunduliwa kwa kijana mwenye umri wa miaka mitano na virusi .

Duru sinasem Mvulana huyo, alisema kuwa alisafiri pamoja na mama yake kutoka DRC Jumapili, alifariki Jumanne usiku.

Image result for uganda ebolaZaidi ya wasafiri mia tatu 300 kutoka mataifa tofauti wamechunguzwa tangu serikali imarishe doria.

Kufuatia mlipuko wa Ebola shirika la Afya Duniani likishirikiana na Serikali ya Uganda na mataifa jira inachukua hatua za dharula kuhakikisha hali imethibitiwa.

WHO imesema wahudumu wa afya 4700 wamepewa chanjo ya kuzuia maambukizi na wamejiandaa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.


Dalili za ebola       
·         Homa

·         Kufuja damu

·         Hutabulika baada ya siku ishirini na moja 21
·         Joto jingi mwilini ya Zaidi ya kipimo  cha 38 degree Homa
·         Kichefuchefu na kutapika
·         Kuharisha
·         Vidonda vya koo
·         Kuumwa kichwa
·         Maumivu ya misuli
·         Kusumbuliwa na tumbo
·         Kuchoka
·         Kukosa hamu ya chakula
Kinga
·         Osha mikono na sabuni: Jiepusha na tabia ya kutoosha mikono
·         Jiepushe na hali ya kumkaribia/kumguza mtu aliyeabukizwa virusi vya Ebola
·         Epuka nyama ya pori
·         Epuka miili ya waliofariki kutakana na maabukizi ya Ebola

Mwanzoni mwa Mwezi huu,shirika hilo la afya ulimwenguni lilisema takriban watu 2,000 wameambukizwa ugonjwa huo nchini Congo.  


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni