Jumatano, 27 Aprili 2016

Malaria Kenya


Idadi ya wagonjwa wa  malaria yapungua Kenya

Ugonjwa wa malaria umekuwa ni tisho katika maeneo yenye joto Afrika hususan nchini Kenya.
Image result for malaria mosquito kenyaJambo la kutia moyo ni kwamba  iadadi ya watu wanaougua ugonjwa huu umepungua marudufu kwa miaka sita iliyopita.

Kulingana na tafiti za wizara ya Afya hali hii inatokana na ongezeko la utumiaji viandarua na pia kupata matibabu mapema.Msemaji wa wizara ya afya Elisha Omondi anasema hatua za serikali za kuukabili ugonjwa wa malaria zimezaa matunda.
Hata hivyo sehemu kama vile  jimbo la Siaya linaongoza kwa maambukizi hayo,lakini pia katika kipindi cha mwaka mmoja angalau asilimia 50 ya visa vimekabiliwa.
Majimbo ya Pwani pia yameadhirika lakini hali sio mbaya kama siku za nyuma.
Takwimu sinaonyesha kuwa Malaria iliwaua karibu watu nusu milioni duniani mwaka jana, huku vifo tisa juu ya kumi vikitoka kusini mwa Sahara.
Kenya ni miongoni mwa mataifa ya kusini mwa Jangwa la Afrika ambapo Malaria imeandelea kuangamiza watu lakini hali hii imeimarika  kwa asili mia nane ikilinganishwa na hali ilivyokua miaka sita iliyopita.
Isistoshe, wanawake waja wazito na watoto wako hatarini zaidi na wanatakikana  wanapokea matibabu punde zinapojitokeza dalili za ugonjwa kwani.

Mama Lucy KIbaki

Aliyekuwa mama wa taifa Aaga dunia


Baada ya kifo chake aliyekuwa Mama wa taifa nchini Kenya,watu wa tabaka mbali mbali wameendelea kutakia familia yake afueni,huku wakimumiminia sifa kama mama wenye bidiina aliyewajali wasiojiweza.

Juhudi zake za kuunda muungano wa akina mama wa marais afrika ili kukabiliana na ugonjwa wa ukimwi ni mfano wa mama aliyewajali wengine.

Pia alikuwa mstari wa mbele kuhakikisa maswala na afya ya uzazi imeimarishwa.Aliwatembelea wagonjwa hospitalini na aliyoyaona hasa mazingira mbaya wagonjwa waliokuwemo yalimtamausha.


Alinena kwa hasira na kutaka hatua kali zichukuliwe kwa maafisa wa selikali wafisadi .

Hospitali ya mama Lucy ilijengwa kwa heshima zake na wakaazi wa Embakazi wana sababu kushukuru kwa hayo."ukakamavu wake mama na bidii katika maswala la afya ilifanya sisi tupate hospitali karibu,tunafurahi sana,alisema Monica Wahito .

John Kariuki anasema ,''hospitali ya mama Lucy imekuwa na sifa mbaya ya kutekelezwa kwa waogojwa na jambo hili ni sharti libadilike kwa heshima ya mama Lucy Kibaki.
Alifanya mambo mengi ambayo tutamkumbuka.

Haijabainika alikokuwa akiugua .Kwa muda mrefu wakenya wamekuwa wakitaka kujua hatima yake ,kwani ajaoneka kwa miaka karibu sita.

Mama Lucy amekuwa akiuguakwa muda .Alilazwa katika hospitali moja hapa nchini Kenya hadi alipohamishwa jijini London kwa matibabu ya dharura hadi kufariki kwake hapo jana.

Mola ailaze roho yake mahali pema peponi.