Azimio la afya kwa wote
Kwenye kikao cha ngazi ya juu kuhusu
afya kwa wote, katika Makao Makuu ya Umoja
wa Mataifa jijini New york, Marekani ,Viongozi walitoa hoja kuwa ni muhimu
swala la afya kwa wote lishighulikiwe kwa haraka na wakaridhia lipitishwe rasmi
na baraza kuu.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio
Guterres akihutumu kwenye kikao hicho alisema,ingawa afya ni haki ya kila mtu,
bado nusu ya watu ulimwenguni wanakosa
haki yao ya msingi.

Dk Ghebreyesus akisema Ulimwengu umebakisha
miaka 11 kuyatekeleza majukumu haya mwafaka ya afya.
Aliwapongeza viongozi kwa kuchukua
uamuzi wa kisiasa wa afya kwa wote.
Azimio hilo linakuja siku moja baada ya
Shirika la Afya Duniani (WHO) na washirika wake kuweka mikakati ya kuboresha
kwa mara mbili viwango vya afya kabla ya
mwaka 2030 ili kuhakikisha watu bilioni
5 wasioweza kupata huduma ya afya hawaja achwa nyuma kwenye mpango huu.
Hii ni kuwa haya yakizingatiwa,
hakuna mtu atapata ugumu wa kupata matibabu ya afya kwa kukosa pesa za
kugharamia matibabu.
Pia serikali zinatarajiwa kutekeleza
mipango ya kiafya yenye athari kubwa kupambana na magonjwa na kulinda afya ya
wanawake na watoto.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Bill &
Melinda Gates, Melinda Gates ambaye ni mfadhili mkuu kwenye sekta ya afya
alisema huu ni wakati wa kufanya kazi kwa bidii ili kubadili ahadi hizo kuwa matokeo.
Wafadhili na serikali za nchi zinahitaji
kusonga mbele zaidi kama kawaida ili kusaidia mifumo ya huduma ya afya
inayoshughulikia mahitaji mengi ya watu kwa maisha yao yote, "alisema
Gates.
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ni
miongoni wa viongozi waliohudhuria kikao hiki.
Hapo awali,rais Kenyatta alikutana na
Katibu Mkuu wa umoja wa Mataifa Antonio Guterres.
Kenya ni mojawapo ya nchini inayofanya bidii kuhakikisha afya ya wote imepewa kibao mbele.
Mnamo tarehe 24 Septemba, WHO na
mashirika mengine 11 ya kimataifa, ambayo kwa pamoja huchangia kwa theluthi moja ya msaada wa maendeleo kwa afya,
itazindua Mpango wao wa Global Action wa afya na ustawi kwa wote na kufikia
malengo yanayohusiana na afya ya SDG.
Viongozi wa dunia wataripoti juu ya maendeleo yao kwa Mkutano
Mkuu wa U.N. mnamo 2023.