Ijumaa, 13 Septemba 2019

chanjo ya malaria


Jaribio la chanjo ya malaria

Huku ugonjwa wa malaria ukiwa miongoni mwa magonjwa hatari duniani,mbinu za kuukabili ugonjwa huu zinaendelea kuguduliwa kila uchao.

Hii leo,nchi ya  Kenya itakuwa miongoni mwa nchi tatu barani Afrika zinazozindua majaribio ya chanjo ya kwanza ulimwenguni dhidi ya malaria.

Nchi zingine kuzindua na kushiriki  katika mpango huu ni Ghana na Malawi.

Zaidi ya watoto 300,000 chini ya miaka miwili wanatarajiwa kupewa chanjo hiyo kila mwaka Katika nchi zote tatu.

Chanjo hiyo inayofahamika kama RTS,S ina mchanganyiko wa dawa inayoisaidia mfumo wa kinga mwilini kukabiliana na mbu wanaosababisha malaria.

Hapo awali majaribio madogo yalionyesha kuwa karibu watoto wanne kati ya 10 kati ya umri wa miaka mitano na 17, waliopata dozi zote nne za chanjo hiyo, walilindwa.
Chanjo hii imekuwa ikifanyiwa utafiti kwa zaidi ya miaka 30.

Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) linasema hii inaweza kubadilika mchezo, lakini inasema chanjo hiyo inatakiwa kutumika kwa mbadala na viandarua na pia dawa .
Malaria inaua watu zaidi ya 400,000 kwa mwaka - zaidi ya nusu yao wakiwa  watoto kutoka Afrika ,Jangwa la Sahara.

Waziri wa Afya wa Kenya Bi Cecily kariuki ataongoza taifa kuzidua mpango huu katika jimbo la Homabay.Serikali imesema kuwa mpango huo utajumuishwa katika mpango wa kitaifa wa chanjo.Huku watoto wa umri wa miaka (6)sita,saba (7) na tisa (9)na miezi 24 wakipata chanjo

Majimbo ya Kisumu,Migori,Bungoma,Busia,Siaya,Vihiga,Kakamenga na mombasa yatafaidika katika mpango huu.

Ingawa serikali imechua hatua kukabili malaria ,bado changamoto ziko.
Hivi mrupuku wa malaria uliua watu wanane Baringo.

Malaria huenezwa na kuumwa na mbu aina ya Anofelesi.

Watoto wa umri wa chini ya miaka 5 wako katika hatari zaidi ya kupata malaria.

Dalili za Malaria

homa kali,
kuhara,
kutapika,
kuumwa kichwa,
Kutetemeka na kuumwa mwili mzima.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni