Alhamisi, 26 Mei 2022

menstral day

 

kesho ni siku ya kimataifa ya hedhi duniani .

siku hii inaadhimishwa wakati kukiwa na changamoto chungu nzima hasa la ukosefu wa taulo za hedhi.Swala la hedhi linachukuliwa na jamii kuwa ni jambo ambalo halistahili kujadiliwa kwa uwazi.Pia tamaduni za kiafrika liliona kama ni mwiko kwa mwanamke aliyenahedhi kutangamana na wengine,na kuonekana kama mchafu.hivyo basi wasichana wanapovunja ungo wanaona haya kuzungumza na pia changamaoto jinzi ya kuzipata taulo.Wasichana wengi wanaostahili kuwa shuleni hupotesa muda mwingi nyumbani kila mwezi kutokana na hedhi.pia wanatumia njia ambazo sio salama kujizua wanapokuwa kwenye hedhi.Mashirika ya kijamii yamejitokeza kutoa pedi shuleni ilikuhakikisha wasichana hawakosi huhudhuria masomo,pia elimu kuhusu usafi na hedhi inatolewa. Unyanyapa au kutengwa  wakati wa hedhi pia ni changamoto kwa wanafunzi wengi  na ni muhimu kuelimisha jamii kuwa hili ni jambo la kawaida na halina aibu.

Wasichana wanapokosa hela ya kununua pedi,waohujihuzisha na maswala ya ngono za mapema ili wapate namna ya kupata pedi.swala hili huchangia ndoa za mapema. Suala la kupatikana kwa vifaa vya hedhi nalo limekuwa tatizo kutokana na bei yake kuwa juu lakini siku za karibuni baadhi ya nchi zimepitisha taulo za kike kuwa bure au kuondolewa kodi na ushuru kama njia ya kutokomeza umaskini utokanao na hedhi salama. Siku ya hedhi salama huadhimishwa tarehe 28 mwezi Mei kwa kuwa mzunguko wa hedhi kwa mwezi ni siku 28 na mtu anaweza kutokwa na hedhi kwa wastani wa siku 5 au 7 kila mwezi. 

 

Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus-WHO

Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus ateuliwa kuhudumu kwa muhula wa pili.

WHO Director-GeneralNchi Wanachama wa Shirika la Afaya Duniani(WHO) zimemchagua tena Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus kuhudumu kwa muhula wa pili wa miaka mitano kama Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo. Dk Tedros alichaguliwa kwa mara ya kwanza mnamo 2017.Kuchaguliwa kwake tena kulithibitishwa wakati wa Mkutano wa 75 wa Afya Ulimwenguni huko Geneva,apolikuwa mgombea pekee. 

Dk Tedros akiongea baadaya ya uchanguzi huo,alisema anmefurahi kupewa fursa nyingine kudumu kama Mkurugenzi mkuu wa WHO.Alisema atatekeleza majukumu yake kama inavyohitajika,kushirikiana na mataifa wnanachama,hata kama changamoto ni nyingi. Shirika la afya duniani hushirikiana na nchi wanachama na pia washirika na wadhamini  , ili kuhakikisha dhamira yake ya kuendeleza maswala ya afya, kuhakiki dunia ni salama na kuwahudumia walio hatarini.

Uchanguzi huu unakuja baadaya ya  uchaguzi ulioanza Aprili 2021 wakati Nchi Wanachama zilialikwa kuwasilisha mapendekezo ya wagombeaji wa wadhifa wa Mkurugenzi Mkuu. Bodi ya Utendaji ya WHO, iliyokutana Januari 2022, ilimteua Dk Tedros kuwania muhula wa pili.Mamlaka mapya ya Dkt Tedros itaanza rasmi tarehe 16 Agosti 2022. Mkurugenzi Mkuu anaweza kuteuliwa tena mara moja, kwa mujibu wa kanuni na taratibu za Bunge la Afya Ulimwenguni.

Wakati wa muhula wake wa kwanza, Dk Tedros alianzisha Mabadiliko mapana ya WHO, yenye lengo la kuongeza ufanisi wa Shirika katika ngazi ya nchi ili kukuza maisha ya afya, kulinda watu wengi katika dharura na kuongeza upatikanaji wa afya kwa usawa. Pia aliongoza mwitikio wa WHO kwa janga la COVID-19, milipuko ya Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na athari za kiafya za majanga mengine mengi ya kibinadamu.Pia alijipata pambaya huku Marekani ikimstumu kwa kuegemea upande wa nchi ya Uchina kuhusiana na maswala ya janga la COVID-19.aliyekuwa Rais waMarekani Donald Trump akionya kutatisha msaada kwa shirika hilo.Marekani ni mfadhiri  mkubwa wa WHO.

Kabla ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dk Tedros aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Ethiopia kuanzia 2012-2016 na Waziri wa Afya, Ethiopia kuanzia 2005-2012. Pia aliwahi kuwa mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria; kama mwenyekiti wa Bodi ya Ubia ya Roll Back Malaria (RBM); na kama mwenyekiti mwenza wa Bodi ya Ubia kwa ajili ya Afya ya Mama, Watoto Waliozaliwa na Mtoto.

 

Jumatano, 23 Machi 2022

TB day

Siku ya Kifua Kikuu Duniani

Siku ya Kifua Kikuu (TB) Duniani huamasishwa Machi 24kila mwaka.lengo likiwa kufahamisha umma idadi ya maabukizi,vifo, juhudi za kukomesha janga la TB na binu mpya zinazobuniwa ili kukabiliana na makali ya ugonjwa wa TB. Mnamo Tarehe mwaka wa 1882 Dk Robert Koch alitangaza kwamba amegundua bakteria inayosababisha TB, ambayo ilitoa fursa ya kutambua na kuponya ugonjwa huu.

TB inasalia kuwa moja ya magonjwa hatari zaidi ya kuambukiza ulimwenguni. Kila siku, zaidi ya watu 4100 hupoteza maisha kwa TB na karibu watu 28,000 wanaugua ugonjwa huu unaozuilika na pia kutibika. Juhudi za kimataifa za kukabiliana na TB zimeokoa maisha ya takriban milioni 66 tangu mwaka wa 2000. Hata hivyo, janga la COVID-19 limerudisha nyuma maendeleo ya miaka mingi iliyopatikana katika vita vya kukomesha TB. Kwa mara ya kwanza katika zaidi ya muongo mmoja, vifo vya TB viliongezeka mwaka 2020.

Kauli mbiu ya Siku ya Kifua Kikuu Duniani mwaka huu-2022, ni ‘Wekeza Kukomesha Kifua Kikuu. Okoa Uhai.’ -inawasilisha hitaji la dharura la kuwekeza rasilimali ili kuimarisha mapambano dhidi ya TB na kufikia ahadi za kukomesha TB zinazotolewa na viongozi wa kimataifa. Hili ni muhimu hasa katika muktadha wa janga la COVID-19 ambalo limeweka maendeleo ya kukomesha hatarini, na kuhakikisha ufikiaji sawa wa kinga na matunzo kulingana na msukumo au kauli ya Shirika La Afya Duniani( WHO)wa kufikia Huduma ya Afya kwa Wote.Uwekezaji zaidi utaokoa maisha ya mamilioni ya watu zaidi, na kuongeza kasi ya kukomesha  janga la TB.

Mwaka jana yaani 2021shirika la kimataifa la kufanikisha uwepo wa tiba nafuu duniani, UNITAID linaloratibiwa na shirika la afya afya dunianui, WHO,lilizidua  dawa  mpya ya kukabiliana na TB aina ya Rifapentine ambayo tayari imeanza kutolewa na kutumiwa katika nchi tano zenye kiwango kikubwa zaidi cha TB barani Afrika .nchi hizo ni Ethiopia, Ghana, Kenya, Zimbabwe na Msumbiji. Wakati wa uziduzi huo, mjini Geneva, Uswsi , Msemaji wa UNITAID Herve Verhoosel akizungumza na waandishi wa habari alisema  “UNITAID alisema kuwa tiba hiyo  mpya ni ya gharama nafuu. Tiba mpya gharama yake ni nafuu kwa asilimia 70 kuliko dawa zaa wali. Inaitwa Rifapentine na kwa majadiliano kati ya UNITAID na wadau wake, dawa hii inaweza kupatikana katika nchi zaidi ya 100 kwa gharama ya dola 15 badala ya  dola 45.” 

WHO ilipendekeza matumizi ya tiba hii mpya kwa watu wagonjwa wa Kifua Kikuu kilichofikichika ambao wanaishi na virusi vya Ukimwi, VVU na wagonjwa wengine wenye Kifua Kikuu na wa umri wowote. Utafiti umebaini kuwa wagonjwa wana uwezo mkubwa wa kukamilisha matibabu katika kipindi kifupi. Wagonjwa wa Kifua Kikuu wanaweza kuambukiza ugonjwa huo kwa watu kati ya 10 hadi 15 wanaokaribiana nao kwa mwaka mzima ambapo UNITAID inasema bila tiba sahihi, asilimia 45 ya watu wasio na VVU wenye Kifua Kikuu na watu wenye VVU na Kifua Kikuu wanaweza kufariki dunia. 

licha ya Kifua Kikuu kuwa ugonjwa unaozuilika na kutibika, bado ni moja ya magonjwa hatari zaidi ya kuambukiza ukisababisha vifo vya watu milioni 1.5 kila mwaka wakiwemo watu 250,000 wanaoishi na virusi vya Ukimwi.” 

Maambukizi ya TB 

Inakadiriwa kuwa mwaka 2019, watu wapatao milioni 10 waliambukizwa Kifua Kikuu, idadi ambayo imekuwa ikipungua taratibu mno katika miaka ya karibuni. Katika idadi hiyo milioni 5.7 ni wanaume, milioni 3.2 wanawake na milioni 1.1 ni watoto na idadi kubwa wanaishi katika nchi za kipato cha chini na kati. Kitaifa, nchi  zenye wagonjwa zaidi wa Kifua Kikuu ni India, Indonesia, China, Ufilipino, Pakistani, Nigeria, Bangladesh na Afrika Kusini. 

Tangu kuibuka kwa  Janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 wagonjwa wa TB wamepata changamoto kupata matibabu.Covid-19  limekuwa mwiba katika tiba dhidi ya kifua kikuu kwa kuwa linavuruga utoaji wa huduma za Kifua Kikuu.

Baadhi ya dalili za ugonjwa wa Kifua Kikuu ni kama vile;homa, kupungua uzito, maumivu ya miguu, kukosahamu ya chakula na kukohoa kwa muda mrefu.