Ijumaa, 6 Februari 2015

Tuna uwezo wa kudhibiti saratani: WHO

 

Tunapo adhimisha siku ya saratani,ugonjwa huu enaenea kwa kasi,lakini jambo la kufurahisha ni kuwa unaweza kudhibitiwa.

Maadhimisho  ya mwaka huu yanaangazia mbinu zinazotumiwa na shirika la afya ulimwenguni, WHO kupunguza mzigo wa ugonjwa huo unaosababisha vifo vya watu Milioni Nane duniani kote kila mwaka. 


WHO inasema kuna nyendo thabiti duniani zinazochochea ongezeko la visa vya saratani hususan kwenye nchi za vipato vya kati na chini ikiwemo uzee, ukuaji holela wa miji na mifumo ya maisha isiyo ya kiafya.

Hata hivyo WHO kupitia ujumbe wa mwaka huu Hauzidi uwezo wetu, inasema jitihada za pamoja zinaweza kudhibiti kitisho hicho kama anavyosema Nelly Enwerem-Bromsom wa mpango wa matibabu ya saratani kutoka shirika la nishati ya atomiki duniani, IAEA.

Bromsom anadokesa kuwa kuna haja  kama jamii ya kimataifa  kama jamii ya kimataifa kuungana kupitia teknolojia bunifu, uchangiaji wa fedha na kushirikiana kukabili mzigo wa ugonjwa huu wa saratani,unaoua zaidi ya wagonjwa Milioni Tano kila mwaka kwenye nchi zinazoendelea. Idadi hii ni zaidi ya wale wanaofariki dunia kwa Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria."


Saratani ya ini imetajwa kuwa tishio zaidi, kwani idadi ya wagonjwa wanaougua saratani ya ini imeongezeka marudufu.
Nchi ya kenya imepiga hatua kuhakikisha mikakati ifaayo imezingatiwa ilikuukabili unonjwa huu hatari.

kwa mujibu wa wizara ya afya Kenya, ni sharti vituo zaidi kuziduliwa mashinanini na pia mashine za kisasa kununuliwa ili kugundua saratani mapewa.
saratani inapogunduliwa mapema huwa inaweza tibiwa na mgonjwa akapona,kuliko wakati mgojwa nanpoenda hospitalini wakati imeenea.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni