Ugonjwa
wa kupooza
Polio
ni ugonjwa unaopooza viungo endapo mtoto hatapata chanjo .Vifo pia hutokea.
Kulingana
na kauli ya mashirika ya afya na hasa lile la Afya Duninani (WHO)ni haki ya
kila mtoto kupata matibabu yafaayo.Chanjo ya polio ikiwa mojawapo.
Kutofanya
hivyo basi kunachukuliwa kama kuvunja sheria na hatua za kiseria zinaweza
kuchukuliwa kwa yeyote.
Hata
hivyo,nchini Kenya kumekuwa na utata kuhusu uharisi wa chanjo hii ya polio.
Wataalamu
wa afya wanaokutoa ushauri kwa kanisa katoliki wameonya kuwa chanjo hii
inachemikali ambazo zinaweza kudhuru afya ya uzazi kwa watoto hao baadaye.
Daktari
Stephen Karanja anayewakilisha kanisa katoliki anasema kuwa aliwasiliana na
wizara ya afya nchini ,lakini maoni au malalamiko yao hayakushughulikiwa.
Anasema
kuwa walifanya utafiti na kugundua kuwa
kuna madini ambayo ina madhara ya baadaye.Watoto
hawa wataadhirika kwenye viungo vyao vya kizazi na hivyo kuwa vigumu kupata
uzazi.
|”maradhara
haya yataonekana baada ya miaka kumi na tano” asema daktari Karanja.
Lakini
kwa upande wake,serikali inapinga madai haya nakusisitisha kuwa hakuna haja ya kutoa
tisho kwa wananchi,”hii chanjo haina madhara yeyote huu ni uvumi tu”,matamshi
yake mkurugenzi wa huduma za afya Kenya,Dkt Nicholas Muraguri.
Anasema
kuwa chanjo hiyo haina homoni ambayo inaadhiri afya ya uzazi.
Chanjo
hii inatolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) na shirika la watoto na elimu
duniani(UNICEF) imepokea tetesi sawa huko Nigeria hapo awali.
Mwaka
2003,viongozi wa kanisa na wale wa siasa walitangaza kuwa chanjo ya polio
ilikuwa ni tishio kwa maisha ya watoto huko kano,zamfara na kaduna kaskazini
mwa nchi ya Nigeria.
Kufuatia
wito kususia chanjo ,mkurupuko wa polio uliripotiwa na maafa zaidi ya 600
katika nchi hiyo na maabukizi kwenye nchi jirani.
Dkt Karanja,,gaenokologia |
Wakati
tetesi kama hizo zinapoibuka wananchi huwa na
hasira na wanaotoa huduma hiyo.visa vya masabulizi yameripotiwa katika vituo
tofauti nchini na pia afrika kwa jumla.
Zaidi
ya hayo,mwaka 2013,huko Nigeria,
wauguzi tisa waliokuwa wakitoa chanjo waliuawa huko Kano.
Wapiganapo
nyati wawili nyasi ndiyo huumia.Imekuwa ni futa ni kufute kati ya serikali na
kanisa huku wakuumia wakiwa ni watoto
ambayo hawajui ukweli uliko.
Waumini
wa kanisa katoliki wamekataa kupeleka
watoto wao kwa chanjo hiyo wakiwa na imani kuwa kanisa linayoyasema ni ukweli
mtupu.
Nilifanya
mahojiano na baadhi ya akina mama wakikatoliki ambayo wanasema kuwa wanaimani
chanjo ya polio ina kasoro kwani kanisa haliwesi kuwatakia mambaya.
Huku
baadhi wa wananchi wakisusia chanjo wengine waloinekana kuwapeleka watoto wao
bila kujali kuwa kwa kweli kuna kasoro kwenye chanjo hii au ni uvumi tu.
Endapo
kanisa ina uhakika kunashida,ukweil ni kwamba itachukua miaka kumi na tano na
zaidi kujia ni nani anasema ukweli.
Lakini
wadadisi wanasema uamuzi wa kanisa kususia chanjo ni hatati kwani kanisa katoliki
hapa nchini Kenya
ni baadhi ya mashirika yayongoza katika sekta ya afya.
Ni
kwa sababu hii kanisa haliwezi kupuuzwa katika maswala ya afya.
Kanisa
katoliki linamiliki hosptali 58,vituo vya afya 83,zahanati 311 na vituo vya
kutoa masomo ya afya 17 nchini Kenya.
Serikali
pia kupitia mkurugenzi wa afya wanasisitiza kuwa shughuli hiyo ilikuwa na
mafanikio,na waliweza kutoa chanjo kwa kiwango walicho tarajia.
Itakuwa
ni jambo la busara kwa kanisa na serikali kukaa kwa meza ya majadiliano na
kupata suluhu ya dharula ili kuepusha maafa au kupooza kwa watoto wasiokuwa na
hatia