polio(ugonjwa wa kupooza)
Ugonjwa wa kupooza Polio ni ugonjwa unaopooza viungo endapo mtoto hatapata chanjo .Vifo pia hutokea. Kulingana na kauli ya mashirika ya afya na hasa lile la Afya Duninani (WHO)ni haki ya kila mtoto kupata matibabu yafaayo.Chanjo ya polio ikiwa mojawapo. Kutofanya hivyo basi kunachukuliwa kama kuvunja sheria na hatua za kiseria zinaweza kuchukuliwa kwa yeyote. Hata hivyo,nchini Kenya kumekuwa na utata kuhusu uharisi wa chanjo hii ya polio. Wataalamu wa afya wanaokutoa ushauri kwa kanisa katoliki wameonya kuwa chanjo hii inachemikali ambazo zinaweza kudhuru afya ya uzazi kwa watoto hao baadaye. Daktari Stephen Karanja anayewakilisha kanisa katoliki anasema kuwa aliwasiliana na wizara ya afya nchini ,lakini maoni au malalamiko yao hayakushughulikiwa. Anasema kuwa walifanya utafiti na kugundua kuwa kuna madini ambayo ina madhara ya baadaye.Watoto hawa wataadhirika kwenye viungo vyao vya kizazi na hivyo kuwa vigumu kupata uzazi. |”maradhar...