Alhamisi, 21 Julai 2016

Tohara Kenya



Huku baadhi ya kabila nchini Kenya zikiendelea kupasha tohara wasichana,shirika la umoja wa mataifa limetaja kitendo hikikama dhuruma kwa watoto.

Daktari Babatunde Osotimehin ambaye ni Mkurugenzi mkuu wa UNPF ametaja ukeketaji kama kitendo cha unyama na dhuruma kwa mtoto.

Alisema kuna haja ya wadau kutafuta mikakati itakayo hakikisha unyama huu imekomeshwa katika sehemu au mataifa yanaoendelea kutekeleza uovu huu,hasabara la afrika abako takwimu zinaonyesha hali ni mbaya.

Mataifa ya jamhuri za kiislamu,Afrika Mashariki,Magharibi na Kusini ni baadhi ya maeneo ambayo yangali yanakubatia mila na tamaduni potovu za ukeketaji.

Alisema shirika lake linatafuta mikakati na sheria ya kuhakikisha swala hili limekomeshwa kabisa.

Hii ni baada ya muda wa miaka ishirini ambapo mashirika ya kiserikali nay ale ya haki za kibinadamu yakikasifu tabia ya ukeketaji barani Afrika .

TB kenya



Kiwango kikubwa cha  watu wanaogua ugonjwa wa kifua kikuu wamekuwa  wakipatikana  na Virusi Vya Ukimwi.Aidha kuchangia vifo miongoni mwa waadhiriwa.

Juhudi za kupambana na TB na maambukizi ya Ukimwi zinaendelea  barani Afrika hususan nchini Kenya.

Hata hivyo, takwimu zinaonyesha kifua kikuu kama moja wapo wa magonjwa ambukizi yanayosababisha maafa nchini. Kesi za kifua kikuu zimeongezeka Zaidi ya mara tatu katika kipindi cha muongo mmoja uliopita.

Mwaka wa 2015 Zaidi ya watu elfu kumi walifariki kutokana na makali ya TB.

Jimbo la Pwani ya Kenya linaongoza kwa idadi ya maambukizi ya kufua kikuu huku Nairobi,Isiolo,Kisumu na Embu zikifuata.
Vile vile,Majimbo ya Samburu,Tharaka,Turkana na Kirinyaga zina idadi ya azili mia 32 ya maambukizi.

Kenya imekuwa mtari wa mbele kuuthibiti ugonjwa wa Tb lakini changamoto zikiwemo wagonjwa kukataa ktafuta matibabu au kukata kumeza dawa.
ilibidi serikali kuweka mikakati madhubuti kuhakikisha kwa hatua za kisheria zinachukuliwa kwa wanaokataa kumeza dawa.
Hata hivyo kutiwa nguvuni waliokiuka maagizo ya daktari yalikosolewa na wanaharakati wa haki za binadamu.
Hiyo pia ni changamoto kwani sheria au sera za afya na wagonjwa pia sharti kiundwe na kulindwa.

Uganda,Tanzania na Zimbabwe bado zimeonekana kushindwa kukambiliana na tishio la TB

Hivi majuzi,serikali ya Kenya  ilizidua  mradi: mulika TB,Maliza TB kama moja wapo wa juhudi za kutokomesha ugonjwa huu nchini.

Jumatatu, 18 Julai 2016

AIDS CONFERENCE DURBAN 2016

Kongamano la tano la kimataifa kuhusu ukimwi kuanza Afrika Kusini

Kongamano kuhusu ukimwi liaanza  mjini Durban, Afrika Kusini. Mkutano huo wa siku tatu unawaleta pamoja wajumbe na wataalam kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni. Mkutano huo unafanyika wakati ambapo  selikali ya Kenya imejitahidi kukabiliana na makali yake.


 Siku chake zilizopita, wizara ya afya Kenya, ilianzisha sera na kampeini ambayo itawasaidia wanaougua na  wanaofahamu hali yao ya HIV kupata tiba mara moja.Kampeini inayo ;anza sasa pia itawezesha watoto wanaozaliwa na virusi vya HIV kuanza matibabu mara moja.
Kenya unveils national initiative to scale up HIV testing and treatment
 Lakutia moyo ni kwamba  idadi ya maabukizi nchini Kenya imepungua,huku Afrika kusini hasa Durban ambapo mkutano huu unafanyika hali ikiwa sio nzuri.

 Zaidi ya hayo,Utafiti unaonyesha  watu milioni 40 ulimwenguni walioambukizwa virusi vya ukimwi wanatokea barani Afrika.

 Serikali ya kenya imetenga shilingi bilioni 22 kupambana na janga hili la Ukimwi huku shilingi 15,000 zikitengwa kwa kila mgonjwa ili kumwezesha kupata dawa za ARV.

 Hii ni binu mwafaka kwani hali  ya kimaisha kwa waadhirirwa itaimarika maradhufu.

Lengo kuu la mkutano wa Durban ni kutathmni tafiti za  kisayansi kuhusu matibabu, dawa na kuzuia kuenea kwa maambukizi ya ukimwi.
 Mbali na huduma nzuri zinazotolewa na mataita mengi ili kudhibiti ukimwi,Changamoto ya bado zipo. Unyanyapaa miongoni mwa wagonjwa wengi wa ukimwi, Majibu yanapobainisha wana virusi vya ukimwi; hawajui wafanye nini au waanza vipi kutumbia tembe.

Hivyo basi,itakuwa ni jambo la kutia moyo baada ya mkutano wa Capetown kukamilika.
  Wataalam na watafiti wa maswala ya afya , mchango wao utazaa matunda  katika kuboresha huduma za matibabu na kupata mbinu  ya watu wanaoishi na virusi vya HIV na wagonjwa wa ukimwi bila kutengwa.
Kongamano hilo ambali, hufanyika kila baada ya miaka miwili na huwavutia wajumbe takriban 5,000 kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni kote. Wanasayansi, madaktari, watalaam wa afya ya umma na viongozi wa kijamii ni pamoja na wanaohudhuria kongamano hili.

Kongamano la awali lililofanyika Australialilikubwa na husuni na kilio baada ya watafiti wa ukimwi kufariki katika ajali ya ndege.