Alhamisi, 21 Julai 2016

Tohara Kenya



Huku baadhi ya kabila nchini Kenya zikiendelea kupasha tohara wasichana,shirika la umoja wa mataifa limetaja kitendo hikikama dhuruma kwa watoto.

Daktari Babatunde Osotimehin ambaye ni Mkurugenzi mkuu wa UNPF ametaja ukeketaji kama kitendo cha unyama na dhuruma kwa mtoto.

Alisema kuna haja ya wadau kutafuta mikakati itakayo hakikisha unyama huu imekomeshwa katika sehemu au mataifa yanaoendelea kutekeleza uovu huu,hasabara la afrika abako takwimu zinaonyesha hali ni mbaya.

Mataifa ya jamhuri za kiislamu,Afrika Mashariki,Magharibi na Kusini ni baadhi ya maeneo ambayo yangali yanakubatia mila na tamaduni potovu za ukeketaji.

Alisema shirika lake linatafuta mikakati na sheria ya kuhakikisha swala hili limekomeshwa kabisa.

Hii ni baada ya muda wa miaka ishirini ambapo mashirika ya kiserikali nay ale ya haki za kibinadamu yakikasifu tabia ya ukeketaji barani Afrika .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni