TB
Tanzania imepiga hatua mbele, kwa kubuni mbinu ya kuukabili ugonjwa wa kifua kikuu, kwa kuzindua MAABARA jijini Dar es salaam. Mradi huu utakua chini ya usimamizi wa chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine. Ubunifu huu utafanywa kwa kutumia panya buku kupima sampuli za ugonjwa wa kifua kikuu (TB).Inaaminika panya mmoja ana uwezo wa kupima sampuli Mia moja katika muda wa dakika ishirini. Hatua hii imefanyika huku kukiwa na ongezeko la idadi ya wagonjwa wa kifua kikuu Tanzania. Tanzania ni miongoni nchi barani Afrika zenye maambukizi ya juu ya ugonjwa huo na kutumia njia hii katika kupambana na ugonjwa huu itakuwa ni afueni. Wataalamu wanasema kuwa njia ya hapo awali ilitoa uhakika wa sampuli kwa asilimia 20 hadi 60 huko asilimia 40 hawagunduliki na hivyo kuendelea kuambukiza wengine. Daktari Georgies Mgode anasema mradi huo wa kupima vimelea vya kifua kikuu utakutumia panya waliofunzwa. Dk.Mgode, ambaye pia ni meneja wa mradi huu, anafafanua kuwa ...