Jumatano, 24 Julai 2019

Dolutegravir(DTG) dawa ya VVU


Shirika la Afya Duniani (WHO) limependekeza dawa ya Dolutegravir(DTG) katika mapambano yake dhidi ya virusi vya Ukimwi,licha ya dawa hiyo kushukiwa kuwa na madhara kwa akina mama waja wazito.

Pendekezo hili limetolewa siku mmoja baadaya ya shirika hilo ,kuchapisha taarifa inayoonyesha  kuwa mapambano dhidi ya Virusi Vya Ukimwi bado yanaendelea.

Image result for dolutegravir
WHO inapendekeza  matumizi ya Dolutegravir(DTG) kama njia ya kwanza na ya pili ya matibabu  kwa watu wote,wakiwemo akina mama wajawazito na pia wenye uwezo wakupata ujauzito.

Tafiti za awali, zilitia shaka  uwezekano wa kuwepo kwa uhusiano kati ya dawa ya DTG na tatizo linalosababisha watoto kuzaliwa na tundu kwenye uti wa mgongo na ubongo,yaani Spinal bifida.

Tatizo hili hutokea punde tu mama anapopata ujauzito huku akitumia dawa ya DTG.

Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo zilitoa tahadhari dhidi ya matumizi ya dawa ya DTG baadaya ya utafiti uliofanywa nchini Botswana kuonyesha kuwa dawa hiyo ilikuwa na madhara kwa wanawake wajawazito,mwaka uliopita.
Utafiti ulibaini visa vinne vya matatizo hayo kati ya wanawake 426 ambao walipata ujauzito wakati wakitumia dawa hizo za DTG.
Kufuatia utafiti huo,Kenya na  nchi nyingi ziliwashauri wanawake wajawazito na wanawake wanao tarajia kubeba ujauzito, kumeza dawa za efavirenz (EFV) badala ya DTG.
Hata hivyo ,baada ya  majaribio ya kisayansi ya kuchunguza ufanisi na usalama kati ya DTG na EFV barani Afrika, sasa ni dhahiri kuwa  kiwango cha hatari ya kupata tatizo la uti wa mgongo na  ubongo ni ndogo mno kinyume na  ilivyokuwa imekadiriwa hapo awali.
Shirika la Afya Duniani ,inasema kuwa DTG ni dawa ambazo zina ufanisi zaidi, rahisi kumeza na zina madhara machache kuliko dawa zingine ambazo zinatumika kwa sasa.
Katika harakati za kupambana na VVU, nchi zinazo endelea 82 ziliripoti kurudia matibabu ya VVU yanayotumia DTG.
WHO inatia mkazo mapendekezo mapya  yaliyoboreshwa na yanayolenga kusaidia nchi zaidi kuboresha sera za afya.
Kufuatia hayo,WHO imeandaa kikundi cha ushauri wa wanawake wanaoishi na VVU kutoka katika Nyanja mbalimbali ili kutoa ushauri katika masuala ya sera zinazohusiana na afya zao, na  zile za afya ya uzazi. 
DTG ilipendekezwa mnamo Juni 2017 kama dawa mbadala ya wanaougua Ukimwi na ambao hawakupata matokeo mema kwa kutumia dawa ya Efavirenz au zile za ARV.
Kenya ilikuwa nchi ya kwanza  barani Afrika kutumia dawa ya Dolutegravir(DTG).

Jumatano, 17 Julai 2019

chanjo ya polio(polio vaccine)


Maisha ya watoto milioni ishirini yako hatarini kufuatia taarifa za umoja wa mataifa kuwa watoto hawakupata chanjo dhidi ya magonjwa yanayozuilika mwaka wa 2018.

Magonjwa yanayozuilika ni kama vile,ugonjwa wa kupooza surua,Dondakoo na pepo punda.

Takwimu hizi zimetolewa na  shirika la afya dudniani(WHO) kwa ushirikiano na Shirika la watoto duniani (UNICEF).

Huku chanjo asilimia 86% ikitolewa kuokoa maisha ya watoto,bado kiwango kinachotakiwa cha asilimia 95% duniani kote hakijafikiwa.

Tangazo hili la umoja wamataifa linatia hofu huku ikifahamika kuwa mlipuko Zaidi waweza kutokea endapo hali hii haita shughulikiwa ipasavyo.

Shabaha ya kutoa chanjo ni kuimarisha afya ya watoto na kuepusha hatari ya milipuko ya wagonjwa yanayozuilika.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Bwana Tedros Adhanom Ghebreyesus amesisitiza kuwa huduma ya chanjo ni muhimu ili kuzuia milipuko ya magonjwa.

Kiwango cha chanjo kwa watoto wasiopata chanjo hasa ni kutokana na hali ya ukimbizi inayosababishwa na vita nchini mwao.

Nchi hizi ni Afghanistan,Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR,Chad, Congo DRC, Ethiopia, Haiti, Mali, Iraq, Niger, Nigeria, Pakistan, Somalia, Sudan Kusini, Syria na Yemen.

Matokeo haya yanaabatana na hali ilivyo nchini Kenya kuhusiana na chanjo ya ugonjwa wa kupooza na chanjo zingine.Inadaiwa kuna kuna upungufu au ukosefu wa chanjo  hospitalini hasa za umma.

Kumekuwa na tuhuma kuwa wazazi wanalazimika kulipa shilingi elfu nane hadi kumi na mbili katika hospitali za kibinafsi ili watoto wao wapate chanjo wanapozaliwa.

Mtoto anapozaliwa anahija kupewa chajo ya kupooza.Chanjo hii hupewa mtoto kupitia kwa mdomo, dozi tatu, halafu baadaye anadungwa shindano anapotimiza miaka mitatu na nusu.

Kinaya ni kuwa Kenya imekuwa katika mstari wa mbele kufanya kampeni dhidi ya chanjo ya ugonjwa wa kupooza (Polio) katika maeneo tofauti nchini.

Zaidi ya hayo,kampeni nyingine ya Polio inatarajiwa kufanyika katika sehemu kadha,huku watoto 2.6 millioni walio chini ya miaka mitano wakitarajiwa kupata chanjo.

Majimbo yaliolengwa katika kampeini ya chanjo ya Polio ni  Mombasa,Tana River,Lamu,Kilifi,Isiolo,Turkana ,Nairobi,Wajir,Garissa na Mandela.

Mwaka 2018 idadi ya watoto walioshambuliwa kwa ugonjwa wa Surua ilikuwa ni 350,000
Kiwango hiki ni mara mbili ya idadi ya watoto walioshambuliwa katika kipindi cha kwa mwaka 2017.

Henrietta Fore Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF, anasema, kuna haja kwa Jumuiya ya Kimataifa kujizatiti vilivyo kutoa chanjo ya kinga kwa kila mtoto duniani.





Ebola Goma



Ebola Goma

Shirika la Afya Duniani(WHO) litafanya kikao cha dharula hii leo kutathmini hatari ya Ebola nchini Congo.

Mkutano huu unafanyika siku moja, baada ya kifo cha kasisi mmoja aliyefariki baada ya kusafiri Butembo kufanya maombi.

Taarifa inasema mhubiri huyu alizuru eneo la Butembo ambalo ni baadhi ya maeneo yanayokabiliwa na ugonjwa wa Ebola kwa muda.

Katika shughuli zake za maombi aliguza wagonjwa na huenda hapo ndipo alipoabukizwa maradhi hayo makali.

Alirudi Goma huku anaumwa na punde alipoenda kutafuta matibabu kwenye zahanati ,akapatikana na ugonjwa wa Ebola.

Moja kwa moja wataalamu wa afya wakachukua hatua kumsafirisha moja kwa moja hadi Butembo kupokea matibabu ya dharula, lakini kwa bahati mbaya akafariki.

Goma ni mji ulio na idadi ya watu milioni moja ,kwenye pwani ya Ziwa Kivu, karibu na Rwanda. 

Ni mara ya kwanza ugonjwa huu kuripotiwa Goma huku wasiwasi ukitanda katika nchi jirani ya Rwanda.Kuna shughuli nyingi hufanyika kila siku mpakani ,hasa katika mji wa Gishenyi.

Serikali ya Rwanda imesema itakuwa hatua ya dharula mpakani kwa kutoa tahadhari kwa  wananchi wake ili kuepuka kupata ugonjwa wa Ebola.

Mkutano wa leo unatarajiwa kutoa hatua au mikakati itakayofuatwa kuukabili ugonjwa wa Ebola ambao ni tishio nchini Congo na pia nchi Jirani.

WHO inafanya kikao baada ya Mkurugenzi Mkuu , Dkt Ghebreyasus kuzuru Congo kufuatia mripuko wa Ebola katika maeneo ya Butembo na Katwa.

Kwenye taarifa,Dkt Ghebreyesus alitoa hakikisho kuwa Shirika lake litajitahidi kuhakikisha kuwa ugonjwa wa Ebola umekabiliwa.

Takribani wahudhumu wa afya elfu tatu,3000 wamepata chanjo ya Ebola huko Goma.

Zaidi ya watu 1650 wamefariki kutokana na maabuziki ya mapya,huku waabukizi 12 yakiripotiwa kila siku.