Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2019

Dolutegravir(DTG) dawa ya VVU

Picha
Shirika la Afya Duniani (WHO) limependekeza dawa ya Dolutegravir(DTG) katika mapambano yake dhidi ya virusi vya Ukimwi,licha ya dawa hiyo kushukiwa kuwa na madhara kwa akina mama waja wazito. Pendekezo hili limetolewa siku mmoja baadaya ya shirika hilo ,kuchapisha taarifa inayoonyesha   kuwa mapambano dhidi ya Virusi Vya Ukimwi bado yanaendelea. WHO inapendekeza    matumizi ya Dolutegravir(DTG) kama njia ya kwanza na ya pili ya matibabu  kwa watu wote,wakiwemo akina mama wajawazito na pia wenye uwezo wakupata ujauzito. Tafiti za awali, zilitia shaka    uwezekano wa kuwepo kwa uhusiano kati ya dawa ya DTG na tatizo linalosababisha watoto kuzaliwa na tundu kwenye uti wa mgongo na ubongo,yaani Spinal bifida. Tatizo hili hutokea punde tu mama anapopata ujauzito huku akitumia dawa ya DTG. Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo zilitoa tahadhari dhidi ya matumizi ya dawa ya DTG baadaya ya utafiti uliofanywa nchini Botswana kuonyesha kuwa dawa h...

chanjo ya polio(polio vaccine)

Maisha ya watoto milioni ishirini yako hatarini kufuatia taarifa za umoja wa mataifa kuwa watoto hawakupata chanjo dhidi ya magonjwa yanayozuilika mwaka wa 2018. Magonjwa yanayozuilika ni kama vile,ugonjwa wa kupooza surua,Dondakoo na pepo punda. Takwimu hizi zimetolewa na   shirika la afya dudniani(WHO) kwa ushirikiano na Shirika la watoto duniani (UNICEF). Huku chanjo asilimia 86% ikitolewa kuokoa maisha ya watoto,bado kiwango kinachotakiwa cha asilimia 95% duniani kote hakijafikiwa. Tangazo hili la umoja wamataifa linatia hofu huku ikifahamika kuwa mlipuko Zaidi waweza kutokea endapo hali hii haita shughulikiwa ipasavyo. Shabaha ya kutoa chanjo ni kuimarisha afya ya watoto na kuepusha hatari ya milipuko ya wagonjwa yanayozuilika. Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Bwana Tedros Adhanom Ghebreyesus amesisitiza kuwa huduma ya chanjo ni muhimu ili kuzuia milipuko ya magonjwa. Kiwango cha chanjo kwa watoto wasiopata chanjo hasa ni kutokana na hal...

Ebola Goma

Ebola Goma Shirika la Afya Duniani(WHO) litafanya kikao cha dharula hii leo kutathmini hatari ya Ebola nchini Congo. Mkutano huu unafanyika siku moja, baada ya kifo cha kasisi mmoja aliyefariki baada ya kusafiri Butembo kufanya maombi. Taarifa inasema mhubiri huyu alizuru eneo la Butembo ambalo ni baadhi ya maeneo yanayokabiliwa na ugonjwa wa Ebola kwa muda. Katika shughuli zake za maombi aliguza wagonjwa na huenda hapo ndipo alipoabukizwa maradhi hayo makali. Alirudi Goma huku anaumwa na punde alipoenda kutafuta matibabu kwenye zahanati ,akapatikana na ugonjwa wa Ebola. Moja kwa moja wataalamu wa afya wakachukua hatua kumsafirisha moja kwa moja hadi Butembo kupokea matibabu ya dharula, lakini kwa bahati mbaya akafariki. Goma ni mji ulio na idadi ya watu milioni moja ,kwenye pwani ya Ziwa Kivu, karibu na Rwanda.  Ni mara ya kwanza ugonjwa huu kuripotiwa Goma huku wasiwasi ukitanda katika nchi jirani ya Rwanda.Kuna shughuli nyingi hufanyika kila ...