Ebola Goma
Shirika la Afya Duniani(WHO) litafanya
kikao cha dharula hii leo kutathmini hatari ya Ebola nchini Congo.
Mkutano huu unafanyika siku moja,
baada ya kifo cha kasisi mmoja aliyefariki baada ya kusafiri Butembo kufanya
maombi.
Taarifa inasema mhubiri huyu alizuru
eneo la Butembo ambalo ni baadhi ya maeneo yanayokabiliwa na ugonjwa wa Ebola
kwa muda.
Katika shughuli zake za maombi
aliguza wagonjwa na huenda hapo ndipo alipoabukizwa maradhi hayo makali.
Alirudi Goma huku anaumwa na punde
alipoenda kutafuta matibabu kwenye zahanati ,akapatikana na ugonjwa wa Ebola.
Moja kwa moja wataalamu wa afya
wakachukua hatua kumsafirisha moja kwa moja hadi Butembo kupokea matibabu ya
dharula, lakini kwa bahati mbaya akafariki.
Ni mara ya kwanza ugonjwa huu
kuripotiwa Goma huku wasiwasi ukitanda katika nchi jirani ya Rwanda.Kuna
shughuli nyingi hufanyika kila siku mpakani ,hasa katika mji wa Gishenyi.
Serikali ya Rwanda imesema itakuwa
hatua ya dharula mpakani kwa kutoa tahadhari kwa wananchi wake ili
kuepuka kupata ugonjwa wa Ebola.
Mkutano wa leo unatarajiwa kutoa
hatua au mikakati itakayofuatwa kuukabili ugonjwa wa Ebola ambao ni tishio
nchini Congo na pia nchi Jirani.
WHO inafanya kikao baada ya
Mkurugenzi Mkuu , Dkt Ghebreyasus kuzuru Congo kufuatia mripuko wa Ebola katika
maeneo ya Butembo na Katwa.
Kwenye taarifa,Dkt Ghebreyesus alitoa
hakikisho kuwa Shirika lake litajitahidi kuhakikisha kuwa ugonjwa wa Ebola
umekabiliwa.
Takribani wahudhumu wa afya elfu
tatu,3000 wamepata chanjo ya Ebola huko Goma.
Zaidi ya watu 1650 wamefariki
kutokana na maabuziki ya mapya,huku waabukizi 12 yakiripotiwa kila siku.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni