Jumatano, 24 Julai 2019

Dolutegravir(DTG) dawa ya VVU


Shirika la Afya Duniani (WHO) limependekeza dawa ya Dolutegravir(DTG) katika mapambano yake dhidi ya virusi vya Ukimwi,licha ya dawa hiyo kushukiwa kuwa na madhara kwa akina mama waja wazito.

Pendekezo hili limetolewa siku mmoja baadaya ya shirika hilo ,kuchapisha taarifa inayoonyesha  kuwa mapambano dhidi ya Virusi Vya Ukimwi bado yanaendelea.

Image result for dolutegravir
WHO inapendekeza  matumizi ya Dolutegravir(DTG) kama njia ya kwanza na ya pili ya matibabu  kwa watu wote,wakiwemo akina mama wajawazito na pia wenye uwezo wakupata ujauzito.

Tafiti za awali, zilitia shaka  uwezekano wa kuwepo kwa uhusiano kati ya dawa ya DTG na tatizo linalosababisha watoto kuzaliwa na tundu kwenye uti wa mgongo na ubongo,yaani Spinal bifida.

Tatizo hili hutokea punde tu mama anapopata ujauzito huku akitumia dawa ya DTG.

Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo zilitoa tahadhari dhidi ya matumizi ya dawa ya DTG baadaya ya utafiti uliofanywa nchini Botswana kuonyesha kuwa dawa hiyo ilikuwa na madhara kwa wanawake wajawazito,mwaka uliopita.
Utafiti ulibaini visa vinne vya matatizo hayo kati ya wanawake 426 ambao walipata ujauzito wakati wakitumia dawa hizo za DTG.
Kufuatia utafiti huo,Kenya na  nchi nyingi ziliwashauri wanawake wajawazito na wanawake wanao tarajia kubeba ujauzito, kumeza dawa za efavirenz (EFV) badala ya DTG.
Hata hivyo ,baada ya  majaribio ya kisayansi ya kuchunguza ufanisi na usalama kati ya DTG na EFV barani Afrika, sasa ni dhahiri kuwa  kiwango cha hatari ya kupata tatizo la uti wa mgongo na  ubongo ni ndogo mno kinyume na  ilivyokuwa imekadiriwa hapo awali.
Shirika la Afya Duniani ,inasema kuwa DTG ni dawa ambazo zina ufanisi zaidi, rahisi kumeza na zina madhara machache kuliko dawa zingine ambazo zinatumika kwa sasa.
Katika harakati za kupambana na VVU, nchi zinazo endelea 82 ziliripoti kurudia matibabu ya VVU yanayotumia DTG.
WHO inatia mkazo mapendekezo mapya  yaliyoboreshwa na yanayolenga kusaidia nchi zaidi kuboresha sera za afya.
Kufuatia hayo,WHO imeandaa kikundi cha ushauri wa wanawake wanaoishi na VVU kutoka katika Nyanja mbalimbali ili kutoa ushauri katika masuala ya sera zinazohusiana na afya zao, na  zile za afya ya uzazi. 
DTG ilipendekezwa mnamo Juni 2017 kama dawa mbadala ya wanaougua Ukimwi na ambao hawakupata matokeo mema kwa kutumia dawa ya Efavirenz au zile za ARV.
Kenya ilikuwa nchi ya kwanza  barani Afrika kutumia dawa ya Dolutegravir(DTG).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni