Maisha ya watoto milioni ishirini yako
hatarini kufuatia taarifa za umoja wa mataifa kuwa watoto hawakupata chanjo
dhidi ya magonjwa yanayozuilika mwaka wa 2018.
Magonjwa yanayozuilika ni kama vile,ugonjwa wa
kupooza surua,Dondakoo na pepo punda.
Takwimu hizi zimetolewa na shirika la afya dudniani(WHO) kwa ushirikiano
na Shirika la watoto duniani (UNICEF).
Huku chanjo asilimia 86% ikitolewa kuokoa
maisha ya watoto,bado kiwango kinachotakiwa cha asilimia 95% duniani kote
hakijafikiwa.
Tangazo hili la umoja wamataifa linatia
hofu huku ikifahamika kuwa mlipuko Zaidi waweza kutokea endapo hali hii haita
shughulikiwa ipasavyo.
Shabaha ya kutoa chanjo ni kuimarisha afya
ya watoto na kuepusha hatari ya milipuko ya wagonjwa yanayozuilika.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Bwana Tedros Adhanom
Ghebreyesus amesisitiza kuwa huduma ya chanjo ni muhimu ili kuzuia milipuko ya
magonjwa.
Kiwango cha chanjo kwa watoto wasiopata chanjo hasa ni kutokana na
hali ya ukimbizi inayosababishwa na vita nchini mwao.
Nchi hizi ni Afghanistan,Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR,Chad, Congo DRC,
Ethiopia, Haiti, Mali, Iraq, Niger, Nigeria, Pakistan, Somalia, Sudan Kusini,
Syria na Yemen.
Matokeo haya yanaabatana na hali ilivyo
nchini Kenya kuhusiana na chanjo ya ugonjwa wa kupooza na chanjo zingine.Inadaiwa kuna kuna upungufu au ukosefu wa chanjo hospitalini hasa za umma.
Kumekuwa na tuhuma kuwa
wazazi wanalazimika kulipa shilingi elfu nane hadi kumi na mbili katika
hospitali za kibinafsi ili watoto wao wapate chanjo wanapozaliwa.
Mtoto anapozaliwa anahija kupewa chajo ya
kupooza.Chanjo hii hupewa mtoto kupitia kwa mdomo, dozi tatu, halafu baadaye
anadungwa shindano anapotimiza miaka mitatu na nusu.
Kinaya ni kuwa Kenya imekuwa katika mstari
wa mbele kufanya kampeni dhidi ya chanjo ya ugonjwa wa kupooza (Polio) katika
maeneo tofauti nchini.
Zaidi ya hayo,kampeni nyingine ya Polio
inatarajiwa kufanyika katika sehemu kadha,huku watoto 2.6 millioni walio chini
ya miaka mitano wakitarajiwa kupata chanjo.
Majimbo yaliolengwa katika kampeini ya
chanjo ya Polio ni Mombasa,Tana
River,Lamu,Kilifi,Isiolo,Turkana ,Nairobi,Wajir,Garissa na Mandela.
Mwaka 2018 idadi ya watoto walioshambuliwa kwa ugonjwa wa Surua ilikuwa
ni 350,000
Kiwango hiki ni
mara mbili ya idadi ya watoto walioshambuliwa katika kipindi cha kwa mwaka 2017.
Henrietta Fore Mkurugenzi Mtendaji wa
UNICEF, anasema, kuna haja kwa Jumuiya ya Kimataifa kujizatiti vilivyo kutoa
chanjo ya kinga kwa kila mtoto duniani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni