Alhamisi, 29 Agosti 2019

Augmentin bandia

Image result for augmentin
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya dhidi ya matumizi ya dawa bandia ijulikanayo kama  Augmentin,nchini Kenya na Uganda.
Shirika hilo limetoa tahadhari wakati kukiwa na ongezeko la ununuzi wa dawa bila ushauri wa wataalam wa afya nchini Kenya.
 WHO imewataka wakenya wawe waangalifu dhidi ya dawa hiyo bandia ya (antibiotic) inayoamikika kuuziwa wagonjwa katika sehemu mbalimbali za nchi.
Augmentin,ni dawa ambayo hutumika dhidi ya maambukizi ya vidudu mwilini na imeorodheshwa na WHO kama mojawapo ya dawa muhimi na inapatikana kwa urahisi katika maduka ya dawa.
Kwenye taarifa yake kwa umma, WHO imesema dawa bandia ina muonekano unaokaribiana sana na dawa halisi inayotengenezwa na kampuni ya madawa ya GlaxoSmithKline (GSK).
Dawa hizo bandia zilibainika baada ya  utafiti wa kukagua ubora wa dawa za antibiotic zinazouzwa kwa wagonjwa.
Baada ya vipimo kwenye maabara za kudhibiti ubora ilibainika kuwa baadhi ya dawa ya Augumentin hazikuwa na viungo muhimu vinavyohitajika na vilivyo kwemye mifuko yake ya upakiaji na pia mandishi.
Dawa bandia zinaweza kusababisha madhara makubwa mwilini,ingawa hadi kwa sasa hakuna aliyeipoti hayo,ingawa kuna wale wanaweza kuwa wameona mabadiliko wanapotumia dawa hii nawasijue ni madhara ya dawa bandia.
Serikali ya Kenya kwa muda mrefu imewaonya wananchi dhidi ya kununua dawa kwa maduka ya dawa bila kibali za daktari.Pia kuna maduka ya madawa yaliyopigwa marufuku kwa kuuza madawa bila lesheni,huku ikiaminika huwa wanauza dawa bila ujuzi elimu  unaostahili kutekeleza majukumu haya.
Hii ni mara ya mbili tahadhari dhidi ya dawa hii kutolewa na WHO barani Afrika.
Tahadhari ya kwanza juu ya uwepo wa dawa hizo bandia ilitolewa mwanzoni wa mwaka huu 2019.
Kampuni ya madawa ya GlaxoSmithKline imesema haihusiki kwenye utengenezaji wa   dawa hizo bandia

Jumatano, 7 Agosti 2019

breastfeeding week


Huku dunia ikiadhimisha wiki ya kimataifa ya kunyonyesha mtoto kuna changamoto kibao ambazo zinazokumba akina mama katika shughuli za kuhakikisha mtoto amenyonya.

Itafahamika kuwa maziwa ya mama yana faida kwa kukua kwa mtoto ikwemo umarishaji wa akili katika maendeleo ya mtoto pia inalinda mtoto dhidi ya magojwa.

Aidha,inalinda akina mama wanaonyonyesha dhidi ya saratani ya shingo ya uzazi na matiti.
Image result for breastfeed africaKatika miji ilioendelea watoto hawanyonyeshwi kulingana na mapendekezo ya Shirika la Afya Duniani (WHO) linalosizitisha kuwa mtoto anastahili kunyonyeshwa  kutoka saa moja anapozaliwa hadi anapofikisha miezi sita.Watoto wa umri huu wanategemea maziwa ya mama pekee.
Hali ni tofauti kwa kiwango cha juu katika maeneo ya mashambani,kwani akina mama wanaoishi maeneo hayo  wanajikakamua kuhakikisha watoto wangenyonyeshwa kikamilifu.
Zaidi ya hayo, shirika la WHO linasema kuwa zaidi ya maisha ya watoto 800 000 walio na umri wa chini ya miaka 5 yanaweza kunusurika kila mwaka, endapo wangenyonyeshwa inavyostahili.

Pia inakadiliwa kuwa kunyonyesha mfurulizo kunaepusha vifo vya wanawake wajawazito 20,000 wanaofariki kutokana na saratani ya titi.

Kulingana na shirika la UNICEF,karibu asili mia watoto 60 hawanyonyeshwi katika miezi sita ya mwanzo iliyopendekezwa na WHO.

Changamoto

·         Kutotenga  seheme za kunyonyesha katika maeneo ya kazi
·         Likizo kwa akina mama wanaonyonyesha na walioajiriwa hazipo.
·         Ukosefu wa lishe bora na kadhalika.

Hata hivyo nchicni Kenya hali inaripotiwa kuimarika ,huku wanawake wengi wakinyonyesha watoto wao kama inavyopendekewa na WHO. 

Kadhalika ,mikakati imewekwa kuhakikisha elimu ya unyonyeshaji imefika kwenye vituo vya huduma ya afya kote nchini.

Jumanne, 6 Agosti 2019

Dkt. Sobbie Mulindi aaga dunia


Dkt. Sobbie Mulindi
Saratani imepokonya nchi ya Kenya Mtafiti wa Virusi Vya Ukimwi na mhadhiri mwandamizi katika idara ya magonjwa ya akili ya Chuo Kikuu cha Nairobi,Dkt Sobbie Mulindi.

Hadi kifo chake hiyo jana,Dkt. Mulindi alikuwa mashuhuri katika janja ya afya.

Ustadi na ukakamavu wake wa utafiti na elimu ya kupunguza maambukizi ya VVU/IKIMWI ulijulikana sio Kenya tu lakini Afrika na dunia yote kwa jumla.

 Pia Mulindi alikuwa Naibu Mkurugenzi wa zamani wa Baraza la Udhibiti wa Ukimwi la Taifa (2008-2014)
Dk Sobbie Z. A. Mulindi alianza masomo yake katika Chuo Kikuu cha Nairobi, na baadaya akawa mkufunzi kwenye chuo hiko.

Zaidi ya hayo,alitumika katika hospitali kuu ya Kenyatta na katika Hospitali ya wagonjwa wa kiakili ya Mathari kufuatia uzoefu kwake katika nyanja ya wagonjwa na kiakili yaani maswala ya kisaikolojia.

Amekuwa mhadhiri katika chuo cha Nairobi kwa zaidi ya miaka 30

Isitoshe,alishiriki katika kukuza Mikakati ya Kitaifa ya kuzuia VVU / UKIMWI nchini Kenya na nchi zingine ikijumuisha Afrika Kusini, Swaziland, Rwanda, Benin, Somali, Kongo  Brazzaville.

Alishiriki kikamilifu kuwapa ushauri wahanga wa milipuko kama vile Bomu jijini Nairobi ,uliotokea Agosti 7, 1998, na mashambilishi ya kigaidi ya Westgate ya mwaka wa 2013.

Pia aliongoza Timu za Ushauri wa Matibabu kwa waadhiriwa wa ajari za ndege ya Kenya huko Abidjan Cote d'Ivoire mwaka wa  2000 na ile ya Duala Cameroon mwaka wa  2007.

Alipokuwa  Mkurugenzi mratibu wa mipango  ya VVU na UKIMWI,alifanya juhudi  ili kupunguza maambukizi kutoka asilimia 14 hadi asilimia 5.6 hivi sasa.