Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2019

Augmentin bandia

Picha
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya dhidi ya matumizi ya dawa bandia ijulikanayo kama   Augmentin,nchini Kenya na Uganda. Shirika hilo limetoa tahadhari wakati kukiwa na ongezeko la ununuzi wa dawa bila ushauri wa wataalam wa afya nchini Kenya.   WHO imewataka  wakenya wawe waangalifu dhidi ya dawa hiyo bandia ya (antibiotic) inayoamikika kuuziwa wagonjwa katika sehemu mbalimbali za nchi. Augmentin,ni dawa ambayo hutumika dhidi ya maambukizi ya vidudu mwilini na imeorodheshwa na WHO kama mojawapo ya dawa muhimi na inapatikana kwa urahisi katika maduka ya dawa. Kwenye taarifa yake kwa umma, WHO imesema dawa bandia ina muonekano unaokaribiana sana na dawa halisi inayotengenezwa na kampuni ya madawa ya GlaxoSmithKline (GSK). Dawa hizo bandia zilibainika baada ya   utafiti wa kukagua ubora wa dawa za antibiotic zinazouzwa kwa wagonjwa. Baada ya vipimo kwenye maabara za kudhibiti ubora ilibainika kuwa baadhi ya dawa ya Augumentin hazikuwa na viungo muhimu...

breastfeeding week

Picha
Huku dunia ikiadhimisha wiki ya kimataifa ya kunyonyesha mtoto kuna changamoto kibao ambazo zinazokumba akina mama katika shughuli za kuhakikisha mtoto amenyonya. Itafahamika kuwa maziwa ya mama yana faida kwa kukua kwa mtoto ikwemo umarishaji wa akili katika maendeleo ya mtoto pia inalinda mtoto dhidi ya magojwa. Aidha,inalinda akina mama wanaonyonyesha dhidi ya saratani ya shingo ya uzazi na matiti. Katika miji ilioendelea watoto hawanyonyeshwi kulingana na mapendekezo ya Shirika la Afya Duniani (WHO) linalosizitisha kuwa mtoto anastahili kunyonyeshwa  kutoka saa moja anapozaliwa hadi anapofikisha miezi sita.Watoto wa umri huu wanategemea maziwa ya mama pekee. Hali ni tofauti kwa kiwango cha juu katika maeneo ya mashambani,kwani akina mama wanaoishi maeneo hayo  wanajikakamua kuhakikisha watoto wangenyonyeshwa kikamilifu. Zaidi ya hayo, shirika la WHO linasema kuwa zaidi ya maisha ya watoto 800 000 walio na umri wa chini ya miaka 5 yanaweza k...

Dkt. Sobbie Mulindi aaga dunia

Picha
Dkt. Sobbie Mulindi Saratani imepokonya nchi ya Kenya Mtafiti wa Virusi Vya Ukimwi na mhadhiri mwandamizi katika idara ya magonjwa ya akili ya Chuo Kikuu cha Nairobi,Dkt Sobbie Mulindi. Hadi kifo chake hiyo jana,Dkt. Mulindi alikuwa mashuhuri katika janja ya afya. Ustadi na ukakamavu wake wa utafiti na elimu ya kupunguza maambukizi ya VVU/IKIMWI ulijulikana sio Kenya tu lakini Afrika na dunia yote kwa jumla.   Pia Mulindi alikuwa Naibu Mkurugenzi wa zamani wa Baraza la Udhibiti wa Ukimwi la Taifa (2008-2014) Dk Sobbie Z. A. Mulindi alianza masomo yake katika Chuo Kikuu cha Nairobi, na baadaya akawa mkufunzi kwenye chuo hiko. Zaidi ya hayo,alitumika katika hospitali kuu ya Kenyatta na katika Hospitali ya wagonjwa wa kiakili ya Mathari kufuatia uzoefu kwake katika nyanja ya wagonjwa na kiakili yaani maswala ya kisaikolojia. Amekuwa mhadhiri katika chuo cha Nairobi kwa zaidi ya miaka 30 Isitoshe,alishiriki katika kukuza Mikakati ya Kitaifa ya kuzuia VV...