Jumatano, 7 Agosti 2019

breastfeeding week


Huku dunia ikiadhimisha wiki ya kimataifa ya kunyonyesha mtoto kuna changamoto kibao ambazo zinazokumba akina mama katika shughuli za kuhakikisha mtoto amenyonya.

Itafahamika kuwa maziwa ya mama yana faida kwa kukua kwa mtoto ikwemo umarishaji wa akili katika maendeleo ya mtoto pia inalinda mtoto dhidi ya magojwa.

Aidha,inalinda akina mama wanaonyonyesha dhidi ya saratani ya shingo ya uzazi na matiti.
Image result for breastfeed africaKatika miji ilioendelea watoto hawanyonyeshwi kulingana na mapendekezo ya Shirika la Afya Duniani (WHO) linalosizitisha kuwa mtoto anastahili kunyonyeshwa  kutoka saa moja anapozaliwa hadi anapofikisha miezi sita.Watoto wa umri huu wanategemea maziwa ya mama pekee.
Hali ni tofauti kwa kiwango cha juu katika maeneo ya mashambani,kwani akina mama wanaoishi maeneo hayo  wanajikakamua kuhakikisha watoto wangenyonyeshwa kikamilifu.
Zaidi ya hayo, shirika la WHO linasema kuwa zaidi ya maisha ya watoto 800 000 walio na umri wa chini ya miaka 5 yanaweza kunusurika kila mwaka, endapo wangenyonyeshwa inavyostahili.

Pia inakadiliwa kuwa kunyonyesha mfurulizo kunaepusha vifo vya wanawake wajawazito 20,000 wanaofariki kutokana na saratani ya titi.

Kulingana na shirika la UNICEF,karibu asili mia watoto 60 hawanyonyeshwi katika miezi sita ya mwanzo iliyopendekezwa na WHO.

Changamoto

·         Kutotenga  seheme za kunyonyesha katika maeneo ya kazi
·         Likizo kwa akina mama wanaonyonyesha na walioajiriwa hazipo.
·         Ukosefu wa lishe bora na kadhalika.

Hata hivyo nchicni Kenya hali inaripotiwa kuimarika ,huku wanawake wengi wakinyonyesha watoto wao kama inavyopendekewa na WHO. 

Kadhalika ,mikakati imewekwa kuhakikisha elimu ya unyonyeshaji imefika kwenye vituo vya huduma ya afya kote nchini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni