Huku dunia ikiadhimisha wiki ya
kimataifa ya kunyonyesha mtoto kuna changamoto kibao ambazo zinazokumba akina
mama katika shughuli za kuhakikisha mtoto amenyonya.
Itafahamika kuwa maziwa ya mama yana
faida kwa kukua kwa mtoto ikwemo umarishaji wa akili katika maendeleo ya mtoto
pia inalinda mtoto dhidi ya magojwa.
Aidha,inalinda akina mama wanaonyonyesha
dhidi ya saratani ya shingo ya uzazi na matiti.
Hali ni tofauti kwa kiwango cha juu
katika maeneo ya mashambani,kwani akina mama wanaoishi maeneo
hayo wanajikakamua kuhakikisha watoto wangenyonyeshwa
kikamilifu.
Zaidi ya hayo, shirika la WHO linasema
kuwa zaidi ya maisha ya watoto 800 000 walio na umri wa chini ya miaka 5
yanaweza kunusurika kila mwaka, endapo wangenyonyeshwa inavyostahili.
Pia inakadiliwa kuwa kunyonyesha
mfurulizo kunaepusha vifo vya wanawake wajawazito 20,000 wanaofariki kutokana
na saratani ya titi.
Kulingana na shirika la UNICEF,karibu
asili mia watoto 60 hawanyonyeshwi katika miezi sita ya mwanzo iliyopendekezwa
na WHO.
Changamoto
· Kutotenga seheme
za kunyonyesha katika maeneo ya kazi
· Likizo
kwa akina mama wanaonyonyesha na walioajiriwa hazipo.
· Ukosefu
wa lishe bora na kadhalika.
Hata hivyo nchicni Kenya hali inaripotiwa kuimarika ,huku wanawake wengi wakinyonyesha watoto wao kama inavyopendekewa na WHO.
Hata hivyo nchicni Kenya hali inaripotiwa kuimarika ,huku wanawake wengi wakinyonyesha watoto wao kama inavyopendekewa na WHO.
Kadhalika ,mikakati imewekwa kuhakikisha elimu ya unyonyeshaji imefika kwenye vituo vya huduma ya afya kote nchini.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni