![]() |
Dkt. Sobbie Mulindi |
Hadi kifo chake hiyo jana,Dkt. Mulindi alikuwa mashuhuri katika janja ya
afya.
Ustadi na ukakamavu wake wa utafiti na elimu ya kupunguza maambukizi ya VVU/IKIMWI ulijulikana sio Kenya tu lakini Afrika na dunia yote kwa jumla.
Ustadi na ukakamavu wake wa utafiti na elimu ya kupunguza maambukizi ya VVU/IKIMWI ulijulikana sio Kenya tu lakini Afrika na dunia yote kwa jumla.
Pia Mulindi
alikuwa Naibu Mkurugenzi wa zamani wa Baraza la Udhibiti wa Ukimwi la Taifa
(2008-2014)
Dk Sobbie Z. A. Mulindi alianza masomo yake katika Chuo
Kikuu cha Nairobi, na baadaya akawa mkufunzi kwenye chuo hiko.
Zaidi ya hayo,alitumika katika hospitali kuu ya Kenyatta
na katika Hospitali ya wagonjwa wa kiakili ya Mathari kufuatia uzoefu kwake
katika nyanja ya wagonjwa na kiakili yaani maswala ya kisaikolojia.
Amekuwa mhadhiri katika chuo cha Nairobi kwa zaidi ya
miaka 30
Isitoshe,alishiriki katika kukuza
Mikakati ya Kitaifa ya kuzuia VVU / UKIMWI nchini Kenya na nchi zingine
ikijumuisha Afrika Kusini, Swaziland, Rwanda, Benin, Somali, Kongo Brazzaville.
Alishiriki kikamilifu kuwapa ushauri wahanga wa milipuko kama vile Bomu jijini Nairobi ,uliotokea Agosti 7,
1998, na mashambilishi ya kigaidi ya Westgate ya mwaka wa 2013.
Pia aliongoza Timu za Ushauri wa Matibabu kwa waadhiriwa wa ajari za ndege ya Kenya huko Abidjan Cote d'Ivoire mwaka wa 2000 na ile ya Duala Cameroon mwaka wa 2007.
Pia aliongoza Timu za Ushauri wa Matibabu kwa waadhiriwa wa ajari za ndege ya Kenya huko Abidjan Cote d'Ivoire mwaka wa 2000 na ile ya Duala Cameroon mwaka wa 2007.
Alipokuwa Mkurugenzi mratibu wa mipango ya VVU na UKIMWI,alifanya juhudi ili kupunguza maambukizi kutoka asilimia 14
hadi asilimia 5.6 hivi sasa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni