Shirika la
Afya Duniani (WHO) limeonya dhidi ya matumizi ya dawa bandia ijulikanayo kama Augmentin,nchini Kenya na Uganda.
Shirika hilo
limetoa tahadhari wakati kukiwa na ongezeko la ununuzi wa dawa bila ushauri wa
wataalam wa afya nchini Kenya.
WHO imewataka wakenya wawe waangalifu dhidi ya
dawa hiyo bandia ya (antibiotic) inayoamikika kuuziwa wagonjwa katika sehemu
mbalimbali za nchi.
Augmentin,ni dawa ambayo hutumika dhidi
ya maambukizi ya vidudu mwilini na imeorodheshwa na WHO kama mojawapo ya dawa
muhimi na inapatikana kwa urahisi katika maduka ya dawa.
Kwenye taarifa yake kwa umma, WHO imesema
dawa bandia ina muonekano unaokaribiana sana na dawa halisi inayotengenezwa na
kampuni ya madawa ya GlaxoSmithKline (GSK).
Dawa hizo bandia zilibainika baada
ya utafiti wa kukagua ubora wa dawa za
antibiotic zinazouzwa kwa wagonjwa.
Baada ya vipimo kwenye maabara za kudhibiti
ubora ilibainika kuwa baadhi ya dawa ya Augumentin hazikuwa na viungo muhimu
vinavyohitajika na vilivyo kwemye mifuko yake ya upakiaji na pia mandishi.
Dawa bandia zinaweza kusababisha madhara
makubwa mwilini,ingawa hadi kwa sasa hakuna aliyeipoti hayo,ingawa kuna wale
wanaweza kuwa wameona mabadiliko wanapotumia dawa hii nawasijue ni madhara ya
dawa bandia.
Serikali ya Kenya kwa muda mrefu
imewaonya wananchi dhidi ya kununua dawa kwa maduka ya dawa bila kibali za
daktari.Pia kuna maduka ya madawa yaliyopigwa marufuku kwa kuuza madawa bila
lesheni,huku ikiaminika huwa wanauza dawa bila ujuzi elimu unaostahili kutekeleza majukumu haya.
Hii ni mara ya mbili tahadhari dhidi ya
dawa hii kutolewa na WHO barani Afrika.
Tahadhari ya kwanza juu ya uwepo wa dawa
hizo bandia ilitolewa mwanzoni wa mwaka huu 2019.
Kampuni ya madawa ya GlaxoSmithKline imesema haihusiki kwenye utengenezaji wa dawa hizo bandia
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni