Jumatatu, 18 Mei 2020


Shirika la Afyan duniani linafanya kikao hii leo mjini Geneva kujadili maswala ya COVID 19

Mkutano huu wa siku mbili unaendelea huku Taiwan ikipinga hatua ya kutengwa katika vikao vya baraza la shirika la afya duniani WHO huku ikisema itakuwa ni hasara kutohudhuria kikao hiki ikizingatiwa kuwa imefanikisha juhudi zake za kukabiliana na virusi vya Corona.

Taiwan na nchi nyingine kadhaa zimelitaka shirika hilo kuialika katika mkutano huo unaofanyika moja kwa moja kupitia mitandao.

Haya yanajili huku uhusiano baina ya Uchina na marekani ukiendelea kuzorota.

Hapo awali Marekani ambaye ni muhisani mkuu wa WHO ilitangaza kusimamisha  msaada wake wa kifedha huku nchi hiyo ikilaumu Shirika hilo kwa kushirikiana na kuipendelea Uchina katika harakati zake za kukabiliana na janga la COVID 19.

 Waziri wa Afya na Ustawi wa Taiwan, Chen Shih-Chung amenukuliwa akilaumu hatua ya kutoshirikishwa kwenye baraza la afya la umoja wamataifa.

Taiwan ni nchi ya visiwani katika Asia ya Mashariki upande wa kusini-mashariki wa China ina serikali yake tangu mwaka 1949 lakini Beijing inaiangalia kama sehemu ya nchi yake kufuatia historia ya nchi hizo.
Baadhi ya wanaohudhuria kikao hiki maalum ni marais wa mataifa mbalimbali ya dunia,wataalam wa afya na wageni wengine mashuhuri.

Mkuu wa shirika la Afya Duniani Tedro Adhanom anasema kuwa huu hiki ni kikao muhimu sana tangu  kuzinduliwa  1948.watu zaidi ya elfu 310,000 wamefariki kufuatia maambukizi ya Corona kote duniani huku millioni 4.7 wakiambukizwa hadi sasa.
Baadhi ya waliochangia katika mazungumzo ni Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaposa na waziri wa Afya Kenya ,Mutahi Kagwe .


Ijumaa, 1 Mei 2020

Antonio Guerres -Corona

Corona au COVID-19.

Huku siku ya uhuru wa vyombo vya habari ikiadhimishwa tarehe 3 Mei kote duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wanahabari na wafanyakazi katika vyombo vya habari wana majukumu muhimu katika kusaidia ulimwenguni kusambaza habari ipasavyo kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.

Alisema ni vema serikali kuwapatia nafasi na uhuru waandishi kutekeleza majukumu yao bila hofu,kuingiliwa au kutishiwa.

Siku ya uhuru was waandishi was habari huadhimishwa kila mwaka; maudhui ya mwaka huu ikiwa,uandishi wa habari bila uoga wala upendeleo,.
Tangu mlipuko was COVID 19 wanahabari wamejipata pambaya n'a selikali tofauti kufuatia j'insiste wanavyo ripoti maambukizi ya Corona. 

Hivi majuzi Tanzania ilistumu vikali habari kuwa kuna idadi kubwa ya maambukizi nchini humo. 

Serikali ya Kenya piano ili kashfu taarifa kuwa idadi ya maambukizi ni zaidi kuliko inavyotangazwa n'a selikali.

Wanahabari pia wanahitaji kulindwa wanapoenda kufanya mahojiano na wataalamu wa afya au wenye maambukizi.

Katika shughuli zao za kila siku wao hukabiliana n'a tishio baada ya nyingine n'a ni jukumu la selikali kuwapatia ulinzi hasa wakati huu was janga hili la Corona.

Fauka ya hayo,Bwana Guterres amesema katika vita dhidi ya virusi vya Corona, wanahabari wanaelimisha jamii jinsi ya kuepuka kuambukizwa Corona na kuwa hii italeta tofauti kubwa kupunguza maambukizi n'a kuokoa maisha .

Isitoshe,Guterres amekumbusha kuwa waandishi kuwezeshwa kufanya kazi zao kwa kupewa nafasi n'a mazingira bora.

Augustine Philip Mahiga

Aliyekuwa Waziri wa Sheria, Tanzania, Augustine Philip Mahiga afariki dunia ghafla huko Dodoma.
Rais Pombe Maghufuli ametangaza .