Shirika la Afyan duniani linafanya kikao
hii leo mjini Geneva kujadili maswala ya COVID 19
Mkutano huu wa siku mbili unaendelea huku
Taiwan ikipinga hatua ya kutengwa katika vikao vya baraza la shirika la afya
duniani WHO huku ikisema itakuwa ni hasara kutohudhuria kikao hiki ikizingatiwa
kuwa imefanikisha juhudi zake za kukabiliana na virusi vya Corona.
Taiwan na nchi nyingine kadhaa zimelitaka
shirika hilo kuialika katika mkutano huo unaofanyika moja kwa moja kupitia
mitandao.
Haya yanajili huku uhusiano baina ya Uchina na
marekani ukiendelea kuzorota.
Hapo awali Marekani ambaye ni muhisani mkuu wa
WHO ilitangaza kusimamisha msaada wake wa kifedha huku nchi hiyo
ikilaumu Shirika hilo kwa kushirikiana na kuipendelea Uchina katika harakati
zake za kukabiliana na janga la COVID 19.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Taiwan, Chen
Shih-Chung amenukuliwa akilaumu hatua ya kutoshirikishwa kwenye baraza la afya
la umoja wamataifa.
Taiwan ni nchi ya visiwani katika Asia ya Mashariki
upande wa kusini-mashariki wa China ina
serikali yake tangu mwaka 1949 lakini Beijing inaiangalia kama sehemu ya nchi
yake kufuatia historia ya nchi hizo.
Baadhi ya wanaohudhuria kikao hiki maalum ni marais wa mataifa mbalimbali ya dunia,wataalam wa afya na wageni wengine mashuhuri.
Mkuu wa shirika la Afya Duniani Tedro Adhanom anasema kuwa huu hiki ni kikao muhimu sana tangu kuzinduliwa 1948.watu zaidi ya elfu 310,000 wamefariki kufuatia maambukizi ya Corona kote duniani huku millioni 4.7 wakiambukizwa hadi sasa.
Baadhi ya waliochangia katika mazungumzo ni Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaposa na waziri wa Afya Kenya ,Mutahi Kagwe .
Baadhi ya wanaohudhuria kikao hiki maalum ni marais wa mataifa mbalimbali ya dunia,wataalam wa afya na wageni wengine mashuhuri.
Mkuu wa shirika la Afya Duniani Tedro Adhanom anasema kuwa huu hiki ni kikao muhimu sana tangu kuzinduliwa 1948.watu zaidi ya elfu 310,000 wamefariki kufuatia maambukizi ya Corona kote duniani huku millioni 4.7 wakiambukizwa hadi sasa.
Baadhi ya waliochangia katika mazungumzo ni Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaposa na waziri wa Afya Kenya ,Mutahi Kagwe .
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni