Alhamisi, 18 Juni 2020

dawa ya dexamethasone -corona


Virusi vya Corona na dawa ya dexamethasone 



Ni avueni kwa  wagonjwa wa COVID 19 baada ya Shirika la Afya Duniani(WHO) kukaribisha matokeo yanayoonyesha kuwa dawa ya dexamethasone inaweza kutibu na kuokoa maisha ya wagonjwa mahututi wanaougua COVID 19 au Corona.
Koronaavaayirasii fi Qoricha: 'Dexamethasone' qoricha akkamiiti ...
Mkurugenzi mkuu wa shirika la Afya Duniani (WHO),Dkt.Tedros Ghebreyesus anasema  utafiti huu ulifanyiwa Uingereza ambapo ,wagonjwa wa Corona waliohitaji Oksijeni na kapewa dawa hii,mmoja kati ya watano alipona.Pia waliokuwa kwenye mashine ya kusaidi kupumua walipopewa dawa ya dexamethasome,mmoja kati ya watatu alipona.

Akizungumza na wanahabari mjini Gevena,Uswisi,Dkt.Ghebreyesus alisema dawa hii imekuwepo kwenye orodha ya WHO ya dawa muhimu tangu miaka ya sabini na inapatikana kwa bei nafuu katika mataifa mengi duniani.

Dexamethasome ni dawa ambayo imekuwa ikitumika tangu 1960.matumishi yake yakiwa ni pamoja na kupunguza uvimbe katika maradhi tofauti mwingine ikiwemo ugonjwa wa saratani.

Wataalamu wa afya wanasisitiza kuwa dawa hii itumiwe chini ya uangalizi mkubwa wa kimatibabu,kwani ina nguvu sana.Inatunika hasa kwa magonjwa mahututi na wanaopata matatizo ya mapavu na uvimbe katika sehemu ya mzunguko wa mapavu na moyo.

Isitoshe,dawa hii inaadhari zake:

  • Kukosa usingizi
  • Kuvuja kwa damu
  • Kutoona vizuri
  • Kuongezeka kwa uzito mwilini

Kulingana na takwimu za Shirika la Afya Duniani(WHO) watu Zaidi ya 5,000 wamefariki kutokana na COVOD 19 kwenye bara la Afrika

Ugonjwa huu unawashabuliwa kwa hali ya juu waliona maradhi mengi tayari,kama vile kisukari,ugonjwa wa moyo na ugonjwa wa presha.


Kenya

Huku hayo yakijiri,Serikali ya kenya imetoa onyo dhidi ya matumuzi ya dexamethasone kwa
wakenya hasa kwa sababu ya madhara yake.
vya COVID 19 vimeongezeka hadi 184, ambavyo ni vya juu zaidi kuripotiwa nchini
hii leo. Vifo vya korona sasa vimefika 107 baada ya watu wawili kufariki.





Jumatatu, 15 Juni 2020

Covid-19 Ikulu Kenya


COVID 19 yabisha hodi Ikuu Kenya

Wafanyakazi wanne wa Ikulu ya rais nchini Kenya wamepatikana na virus vya corona hayo yemedhibitishwa na  msemaji wa Ikulu Kanze Dena.
Dena amesema kuwa wafanyakazi hao waligunduliwa kuaambukizwa COVID-19 baada ya kufanyiwa uchunguzi Alhamisi wiki iliyopita.
Wakanyikazi hayo wa ikulu wanaendelea kupokea matibabu katika Hospitali ya rufaa ya Chuo Kikuu cha Kenyatta.
Zaidi ya hayo,Bi Dena amewahakikishia Wakenya kuwa Rais Kenyata na familia yake wake wako salama salimini na wamepatikana kutokuwa  na maambukizi ya corona.
Hii ni ishara kuwa kila mtu yuko katika hatari ya kuambukizwa Corona endapo hatua zilizowekwa na Shirika la Agya Duniani na Wizara ya Afya hayatazingatiwa.
Kuvaa barakoa, kuosha mikono na maji yanayotiririka na kujiepunga/kujitenga na sehemu ambapo kuwa umati ni baadhi ya masharti ya kuzingatiwa.
Ikulu pia imehakikisha kuwa ili kuzuia maambukizi ya Corona kuenea , wafanyakazi wote wanaoishi nje ya Ikulu pamoja na wageni wamedhibitiwa huku masharti ya wizara ya afya yakiendela kutekelezwa.
Jana waziri wa Afya ,Mutahi kagwe alitangaza kuwa idada ya watu, walioambukizwa virusi vya corona imeongezeka hadi 3,727.
Waziri wa Afya Mutahi Kagwe, amesema  pia kuna ,jumla ya 1286  waliopona katika kipindi cha saa 24.
Hata hivyo ,waziri amewataka wakenya kuendelea kufuata mikakati iliyowekwa na serikali ilikukabiliana na janga hili.


Jumatano, 10 Juni 2020

Rais Pierre Nkurunziza -kifo


Mke wa Rais wa Burundi aendelea kupata matibabu huku mumewe akiombolezwa

Huku warundi na watu watabaka mbalimbali wakiendelea kuomboleza kifo cha aliyekuwa Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza,Mkewe angali anapokea matibabu nchini kenya kutokana na kile kinachotajwa kama maaambukizi ya virusi vya Corona.

Bi Denise Nkurunziza amekuwa Nairobi kwa wiki mbili sasa,akiwa amelazwa katika hospital ya Agah Khan na matatizo ya kupumua ,ingawa hospitali hiyo imekataa kutoa taarifa ya anapoumwa Bi Nkurunziza.

Burundi: Perezida Pierre Nkurunziza yaryamiye ukuboko kw'abagabo ...Kabla ya kuhamishiwa Kenya kwa matibabu,uvumi ulienea ndani na nje ya Nchi ya Burundi kuwa Mke wa Rais alikuwa kaambukizwa virusi vya Corona na alikuwa katika hali mahututi.
Kuligana na hali yake ya kiafya,Bi Nkurunziza alisafirishwa nchini Kenya na Ndege ya shirika la Afya la AMREF .

Mwenda zake Rais Nkurunziza anadaiwa kufariki baada ya msituko wa moyo huku uvumi uliokuwa ukienea nchini kuwa pia yeye alikuwa akiugua virusi vya Corona kukipigwa.

Taarifa ya serikali ya Burundi iliyotolewa kwa umma inadhibitisha kuwa amefariki kutokana na mshtuko wa moyo.
Rais Nkurunziza ametawala Burundi kwa miongo mitatu yaani miaka kumi na tano na amefariki siku chache baada ya uchanguzi wa nchi hiyo,ambapo Generali Evariste Ndayisimiye alitangazwa mshindi wa uchaguzi huyo.

Nkurunziza alitalajiwa kumkabidhi mamlaka Rais huyo mteuliwa mwezi wa nane ,mwaka huu.
Serikali ya Burundi imetanga maobolezi ya kitaifa huku bendera ya nchi hiyo ikipeperushwa nusu mlingoti.

Mola awape afueni wenye majonzi.

Presha au shinikisho la damu

Mshtuko wa moyo unatokea wakati damu inapiga kwa wingi na mishipa ikiwa miyembamba. Watu wengi hufariki ghafla baadha ya mstuko wa moyo. Wataalam wa afya wanasema kuwa hali hii inauwa watu wengi bila kuonyesha dalili huku wakisisitisha umuhimu wa kupimwa mara kwa mara.
Kipimo cha shinikizo la damu kawaida ni 100–140 mmHg kipimo cha juu na 60–90 mmHg kikiwa kipimo cha chini. Shinikizo la juu la damu hutokea kipimo kikiwa zaidi ya 140/90 mmHg kwa muda mrefu.
Ugonjwa huu isipogunduliwa mapewa unaweza kusababisha madhara ya kiafya.