dawa ya dexamethasone -corona
Virusi vya Corona na dawa ya dexamethasone Ni avueni kwa wagonjwa wa COVID 19 baada ya Shirika la Afya Duniani(WHO) kukaribisha matokeo yanayoonyesha kuwa dawa ya dexamethasone inaweza kutibu na kuokoa maisha ya wagonjwa mahututi wanaougua COVID 19 au Corona. Mkurugenzi mkuu wa shirika la Afya Duniani (WHO),Dkt.Tedros Ghebreyesus anasema utafiti huu ulifanyiwa Uingereza ambapo ,wagonjwa wa Corona waliohitaji Oksijeni na kapewa dawa hii,mmoja kati ya watano alipona.Pia waliokuwa kwenye mashine ya kusaidi kupumua walipopewa dawa ya dexamethasome,mmoja kati ya watatu alipona. Akizungumza na wanahabari mjini Gevena,Uswisi,Dkt.Ghebreyesus alisema dawa hii imekuwepo kwenye orodha ya WHO ya dawa muhimu tangu miaka ya sabini na inapatikana kwa bei nafuu katika mataifa mengi duniani. Dexamethasome ni dawa ambayo imekuwa ikitumika tangu 1960.matumishi yake yakiwa ni pamoja na kupunguza uvimbe katika maradhi tofauti mwingine ikiwemo ugonjwa wa s...