Virusi vya Corona na dawa ya dexamethasone
Mkurugenzi mkuu wa shirika la Afya Duniani (WHO),Dkt.Tedros Ghebreyesus anasema utafiti huu ulifanyiwa Uingereza ambapo ,wagonjwa wa Corona waliohitaji Oksijeni na kapewa dawa hii,mmoja kati ya watano alipona.Pia waliokuwa kwenye mashine ya kusaidi kupumua walipopewa dawa ya dexamethasome,mmoja kati ya watatu alipona.
Akizungumza na wanahabari mjini
Gevena,Uswisi,Dkt.Ghebreyesus alisema dawa hii imekuwepo kwenye orodha ya WHO
ya dawa muhimu tangu miaka ya sabini na inapatikana kwa bei nafuu katika
mataifa mengi duniani.
Dexamethasome ni dawa ambayo imekuwa
ikitumika tangu 1960.matumishi yake yakiwa ni pamoja na kupunguza uvimbe katika
maradhi tofauti mwingine ikiwemo ugonjwa wa saratani.
Wataalamu wa afya wanasisitiza kuwa dawa
hii itumiwe chini ya uangalizi mkubwa wa kimatibabu,kwani ina nguvu
sana.Inatunika hasa kwa magonjwa mahututi na wanaopata matatizo ya mapavu na
uvimbe katika sehemu ya mzunguko wa mapavu na moyo.
Isitoshe,dawa hii inaadhari zake:
- Kukosa usingizi
- Kuvuja kwa damu
- Kutoona vizuri
- Kuongezeka kwa uzito mwilini
Kulingana na takwimu za Shirika la Afya
Duniani(WHO) watu Zaidi ya 5,000 wamefariki kutokana na COVOD 19 kwenye bara la
Afrika
Ugonjwa huu unawashabuliwa kwa hali ya
juu waliona maradhi mengi tayari,kama vile kisukari,ugonjwa wa moyo na ugonjwa
wa presha.
Kenya
Huku hayo yakijiri,Serikali ya kenya imetoa onyo dhidi ya matumuzi ya dexamethasone kwawakenya hasa kwa sababu ya madhara yake.
vya COVID 19 vimeongezeka hadi 184, ambavyo ni vya juu zaidi kuripotiwa nchini
hii leo. Vifo vya korona sasa vimefika 107 baada ya watu wawili kufariki.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni