Jumatatu, 15 Juni 2020

Covid-19 Ikulu Kenya


COVID 19 yabisha hodi Ikuu Kenya

Wafanyakazi wanne wa Ikulu ya rais nchini Kenya wamepatikana na virus vya corona hayo yemedhibitishwa na  msemaji wa Ikulu Kanze Dena.
Dena amesema kuwa wafanyakazi hao waligunduliwa kuaambukizwa COVID-19 baada ya kufanyiwa uchunguzi Alhamisi wiki iliyopita.
Wakanyikazi hayo wa ikulu wanaendelea kupokea matibabu katika Hospitali ya rufaa ya Chuo Kikuu cha Kenyatta.
Zaidi ya hayo,Bi Dena amewahakikishia Wakenya kuwa Rais Kenyata na familia yake wake wako salama salimini na wamepatikana kutokuwa  na maambukizi ya corona.
Hii ni ishara kuwa kila mtu yuko katika hatari ya kuambukizwa Corona endapo hatua zilizowekwa na Shirika la Agya Duniani na Wizara ya Afya hayatazingatiwa.
Kuvaa barakoa, kuosha mikono na maji yanayotiririka na kujiepunga/kujitenga na sehemu ambapo kuwa umati ni baadhi ya masharti ya kuzingatiwa.
Ikulu pia imehakikisha kuwa ili kuzuia maambukizi ya Corona kuenea , wafanyakazi wote wanaoishi nje ya Ikulu pamoja na wageni wamedhibitiwa huku masharti ya wizara ya afya yakiendela kutekelezwa.
Jana waziri wa Afya ,Mutahi kagwe alitangaza kuwa idada ya watu, walioambukizwa virusi vya corona imeongezeka hadi 3,727.
Waziri wa Afya Mutahi Kagwe, amesema  pia kuna ,jumla ya 1286  waliopona katika kipindi cha saa 24.
Hata hivyo ,waziri amewataka wakenya kuendelea kufuata mikakati iliyowekwa na serikali ilikukabiliana na janga hili.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni