Uaviaji Mimba
WHO/Picha
Baina ya Haki na Uhalisia: Vikwazo Vinavyo Changia Vifo vya Wanawake Barani Afrika
Kifo Kila Dakika 30
Kila dakika 30, mwanamke mmoja barani Afrika anakufa kutokana na matokeo
ya utoaji mimba usio salama. Kulingana na watafiti vifo hivi vinaweza
kuzuilika kabisa.
Ripoti mpya iliyozinduliwa katika Mkutano wa Kimataifa wa Mipango ya
Uzazi (ICFP) mjini Bogotá — iitwayo “The Maze Women Face: Stuck Between
Rights and Reality” — imefichua pengo kubwa kati ya haki zilizoandikwa
kisheria na hali halisi inayowakabili wanawake na wasichana.
Utafiti huo, unaoongozwa na Chuo Kikuu cha Rutgers na taasisi
washirika za Afrika Magharibi na Kati, umeunganisha moja kwa moja matukio ya unyanyasaji
wa kijinsia na utoaji mimba usio salama, na kufichua jinsi woga,
unyanyapaa, na ukosefu wa huduma vinavyosukuma wanawake katika njia za hatari.
“Tulikutana na wasichana waliobakwa na kujaribu kutoa mimba kwa kutumia
dawa au miti shamba waliyonunua sokoni,” anasema Mena Agbodjavou wa
shirika la CERRHUD nchini Benin. “Wengi waliishia hospitalini wakiwa
mahututi. Hii siyo hadithi ya mtu mmoja, ni hali ya kawaida katika eneo letu.”
Taswila ya Ulimwengu: Haki Zipo,
Lakini Utekelezaji ni
Tatizo
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO, 2023), kuna takribani
utoaji mimba milioni 73 duniani kila mwaka, na asilimia 45% kati
ya hizo ni zisizo salama.
Asilimia 97% ya utoaji mimba usio salama hutokea katika nchi zenye
kipato cha chini au cha kati.
Photo.WHO
- Utoaji
mimba usio salama unachangia takribani asilimia 13 ya vifo vya
wajawazito duniani — zaidi ya 39,000 kila mwaka.
- Barani
Afrika, karibu utoaji mimba 3 kati ya 4 hufanywa katika
mazingira hatarishi.
Kenya: Wakati Sheria Inapokabiliana na Unyanyapaa
Nchini Kenya, katiba inaruhusu utoaji mimba iwapo maisha au afya
ya mama yako hatarini, au kama inaruhusiwa na sheria nyingine iliyoandikwa.
Hata hivyo, upatikanaji wa huduma salama unabaki kuwa ndoto.
Utafiti wa African Population and Health Research Center (APHRC)
mwaka 2012 uligundua kuwa kulikuwa na takriban utoaji mimba 464,690
nchini humo — sawa na kiwango cha 48 kwa wanawake 1,000 wenye umri wa miaka
15–49.
Kati ya hawa, wanawake 120,000 waliishia hospitalini wakiwa na matatizo
makubwa, huku takriban 2,600 wakipoteza maisha kila mwaka.
“Tunapokea wagonjwa wenye majeraha makubwa ya uzazi au maambukizi
makali, wengi baada ya kutumia njia hatarishi,” anasema muuguzi wa afya ya
uzazi katika mtaa wa mabanda Nairobi. “Woga wa hukumu au kukamatwa unawasukuma
wanawake kuficha tatizo.”
Nigeria: Imani, Hofu na
Vifo
Nchini Nigeria, utoaji mimba unaruhusiwa tu ili kuokoa maisha ya
mama. Lakini Shirika la Guttmacher linakadiria kuwa utoaji mimba
milioni 2 hufanyika kila mwaka nchini humo, nyingi zikiwa zisizo salama.
Utafiti uliochapishwa katika The Lancet Global Health unaonyesha
kuwa utoaji mimba usio salama unachangia vifo vya wanawake wasiopungua
10,000 kila mwaka.
Katika mtaa wa Lagos, “Grace,” mwanafunzi wa miaka 23, alibakwa na mmiliki wa nyumba. “Nilinunua dawa kwa ‘pharmacist’ wa mitaani. Nilivuja damu kwa siku kadhaa, sikuweza kwenda hospitalini kwa hofu ya kuulizwa maswali.” Alinusurika, lakini maelfu hawana bahati hiyo.
Ethiopia: Mafanikio
Yanayoleta Tumaini
Nchini Ethiopia, mabadiliko ya sheria mwaka 2005 yaliyojumuisha
utoaji mimba salama ndani ya huduma za afya za umma yamesababisha upungufu
wa vifo vya uzazi kwa asilimia 72 ndani ya miaka kumi. Mafanikio haya
yanaonyesha kwamba sheria pekee haitoshi — inahitaji uwekezaji, elimu, na
ujasiri wa kisiasa.
Athari za Kisiasa: “Global
Gag Rule” ya Trump
Ripoti hii pia inatolewa katika kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu
kuchaguliwa tena kwa Donald Trump, tukio lililobadilisha kwa kiasi
kikubwa ufadhili wa afya duniani. Kupitia sera ya Global Gag Rule,
mashirika yote yanayoshughulika na huduma za uzazi na kujadili utoaji mimba
yalikatwa ufadhili wa Marekani.
Matokeo yake, kliniki nyingi Afrika zilikosa vifaa na wahudumu. Marie Stopes International iliripoti kuwa zaidi ya wanawake milioni 1.5 barani Afrika walikosa huduma muhimu za uzazi kutokana na sera hizo.
Vikwazo
Utafiti wa Rutgers umebainisha mnyororo wa vikwazo vinavyowazuia
wanawake kupata huduma salama:
- Ushahidi
mgumu: Waliobakwa hulazimishwa kuwasilisha ripoti za
polisi au matibabu kabla ya kupata huduma.
- Kutokujua
sheria: Wahudumu wengi hawajui mipaka ya kisheria,
hivyo wanakataa kutoa huduma.
- Urataibu
wa taratibu: Vikwazo vya kiutawala vinachelewesha huduma
hadi hali kuwa mbaya.
- Unyanyapaa:
Hofu ya aibu na hukumu inawafanya wanawake kuficha mimba.
- Ukata
wa fedha: Kupungua kwa ufadhili wa kimataifa
kunapunguza vifaa na mafunzo.
Takwimu kwa Muhtasari
|
Eneo |
Asilimia ya utoaji mimba usio salama |
Vifo vya wajawazito kwa 100,000 (WHO 2023) |
Sababu kuu |
|
Afrika
Kusini mwa Jangwa la Sahara |
77% |
525 |
Sheria
kandamizi, ukosefu wa huduma, unyanyapaa |
|
Amerika
ya Kusini |
75% |
169 |
Sheria
kali, unyanyapaa wa kijamii |
|
Asia
(nchi zinazoendelea) |
49% |
149 |
Ukosefu
wa huduma vijijini, taarifa potofu |
|
Nchi
zilizoendelea |
<1% |
10 |
Upatikanaji
wa huduma salama na nafuu |
Sera Muhimu za Kufuatilia
(2025–2026)
·
Kenya: Wizara ya Afya
inakamilisha mapitio ya Sera ya Afya ya Uzazi (2019–2030) ili kujumuisha
miongozo ya utoaji mimba salama.
·
Benin: Sheria mpya za 2024
zinapanua haki za kutoa mimba, lakini wahudumu bado wanahitaji mafunzo.
·
Nigeria na Ghana:
Mashirika ya kiraia yanapigania uhalalishaji wa utoaji mimba na huduma za baada
ya utoaji mimba.
·
WHO na UNFPA: Zinatekeleza
Mwongozo wa Utoaji Mimba Salama 2022 kusaidia nchi kuboresha sera.
·
Wadau wa Kimataifa:
Mashirika yanahamasisha kurejeshwa kwa ufadhili wa afya ya uzazi uliopotea
kutokana na siasa za Marekani.
Zaidi ya Sheria: Mapambano
ya Kisaikolojia na Kijamii
“Hatuwezi kutunga sheria ya huruma,” anasema Dkt. Jonna Both,
mmoja wa waandishi wa ripoti. “Mpaka tutakapoondoa unyanyapaa hospitalini,
nyumbani, na bungeni, wanawake wataendelea kuteseka kimya kimya.”
Utoaji mimba salama si hoja ya siasa pekee — ni suala la heshima,
uhuru, na haki ya msingi ya kibinadamu.
“Haki bila utekelezaji ni ahadi tupu,” anaandika Both. “Wanawake wanahitaji usalama siyo kwenye karatasi, bali katika maisha yao ya kila siku.”
Maoni
Chapisha Maoni