Jumanne, 26 Februari 2013

Anyang Nyong'o vita dhidi ya saratani

 Saratani

Vita dhidi ya ugonjwa wa saratani umeimarishwa baada ya waziri wa huduma za matibabu ya umma Nyang nyong'o  kutangaza kuwa shirika mmoja la Uingereza limetoa fedha zaidi ya shillingi 517 billion kugharamia ujenzi wa kituo cha saratani nchini Kenya.

Hii ni afueni kwa wakenya hususan wanaougua saratani watapata matibabu bila kusubiri kwa miezi kama hali ilivyo kwa sasa.

Hospitali kuu ya Kenyatta inahudhumia wakenya kutoka sehemu zote za nchi, jambo ambalo linafanya wengi kusubiri kwa miezi tano na zaidi kabla ya kuhudumiwa.

Kulingana na takwimu za afya, wakenya 18,000 hufariki kutokana na maradhi ya saratani kila mwaka.Pia vifaa vinanavyotumiwa kutibu na kuutafiti ugonjwa huu ni duni na vya kiwango cha chini ikilinganishwa na mataifa yalitiyostawi.

Ili kukabiliana na saratani kwa undani, Rais Mwai kibaki mwaka jana alipitisha sheria ya saratani"cancer prevetion Bill 2012 ilikuhakikisha kuwa wanaougua saratani wanapata huduma bora ya afya.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni