Jumanne, 26 Februari 2013

Samuel kivuitu aiaga dunia



Aliyekuwa mwenyekiti  wa iliyokuwa tume ya uchaguzi   ECK Samuel Kivuitu ameaga dunia.

Kivuiti mwenye umri wa miaka 74 amekuwa akiigua saratani ya  koo.
Kwa mujibu wa msemaji wa  familia yake,Mzee Kivuitu amefariki dunia katika hospitali ya MP Shah mjini Nairobi alipokuwa akipata matibabu ya maradhi ya kansa. Taarifa zaidi zinasema, Kivuitu amekuwa akiugua  kwa muda wa miaka miwili sasa.Amekuwa akipokea matibabu ndani na nje ya nchi. Matokeo ya uchaguzi wa rais nchini Kenya mwaka 2007 yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya wakati huo ECK chini ya uwenyekiti wa Samuel Kivuitu yalipelekea kutokea machafuko makubwa kuwahi kushuhudiwa katika historia ya Kenya ambapo watu 1,133 waliuawa na wengine laki sita na nusu kubaki bila makazi.
Kifo cha Kivuitu kimetokea wiki moja kabla ya uchanguzi mkuu unaotarajiwa  kufanyika mapema mwezi ujao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni