world malaria day
siku ya malaria duniani Huku dunia ikiadhimisha siku ya Malaria hii leo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ametoa ujumbe na kusema kuwa bado ugonjwa huo ni tishio kwa nchi maskini hususan barani Afrika, ambako mamilioni ya watu wanashindwa kujikinga dhidi ya Malaria. Isitoshe,Bwana Ban amesema barani Afrika kila dakika mtoto mmoja anafariki dunia kutokana na ugonjwa huo na kwamba mifumo dhaifu ya ufuatiliaji inakwamisha uwezo wa serikali na shirika la afya duniani, WHO kupata taarifa za kina kuhusu maeneo mapya yenye ugonjwa huo na mabadiliko ya mwenendo wa ugonjwa huo. Amesema usugu wa vijidudu vya Malaria dhidi ya dawa za kunywa na hata katika vyandarua vyenye viuatilifu, unafanya hali kuwa mbaya zaidi kuweza kutokomeza ugonjwa huo na hivyo kutishia uhai na maendeleo. Kauli mbiu inayoongoza Maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani kwa Mwaka 2013; Wekeza kwa siku za baadaye. Shinda Malaria. Bwana Ban amesema ameisihi...