Jumatano, 16 Oktoba 2013

 

Saratani tezi

Huku ukiwa mwezi wa kupambana na janga la ugonjwa wa saratani,watu wengi hawapendi  kwenda hospitalini kwa uchunguzi,huku wakihofia kugunduliwa na maradhi ya saratani.
Hii ni baadhi ya sababu zinazopelekea ongezeko la saratani nchini kenya na kanda la afrika kwa jumla.
Inakisiwa kuwa zaidi ya watu elfu moja(1,000)  huugua saratani huku zaidi ya  850 wakifariki kila mwaka.
Takwimu pia zinaonyesha idadi ya saratani ya tezi kibofu inaongezeka marudufu.

Saratani ya tezi kibofu ni ugonjwa ambao  huwa kati ya wanaume.kama aina nyingine za saratani, inapogunduliwa mapema inakuwa ni rahisi kutibiwa. Zaidi ya hayo, walio  hatarini ya kuambukizwa Ugonjwa huu ni  wanaume walio na umri wa miaka 55 na zaidi.

 Kulingana na watalaamu wa afya watu wengi hutafuta tiba wakati ugojwa umeenea zaidi.

Hivi majuzi, ugonjwa wa saratani umetia wengi kiwewe.Siku baada ya siku kuna habari kuwa mtu fulani ana ugonjwa wa saratani.Waume kwa wanawake,vijana  kwa watoto wote wako hatarini ya kuabukizwa ugonjwa huu.

Watafiti bado hawajapata uvubuzi ni nini haswa inayo sababisha ugonjwa huu hatari.

Hata hivyo inakisiwa kuwa  mazingira tunayoishi, kwa njia moja ua nyingine yanachangia kuwepo kwa maradhi haya.

Waziri Mwenzake, Prof. Anyang Nyongo pia aligunduliwa kuugua saratani ya tezi kibofu.Kwa bahati nzuri, iligunduliwa mapema na baada ya matibabu ya muda, madaktari walimhakikishia  kuwa amepona.

Pia mwanahabari mashuhuri Jerry Okungu ana saratabni ya tezi kibofu.Amekuwa akikabiriana na ugonjwa huu kwa muda sasa.Afueni ni kuwa haja kata tamaa na ameanzisha wakfu wa saratani ili kuwaelimisha na kuwasaidia wale wasioweza kugharamia matibabu.

 

Matibabu ya saratani huwa ghali mno,hivyo basi wale wanaougua wanakubwa na matatizo ya kutafuta matibabu,hii huchangia kuzorota kwa afya na hata maafa.

Ugonjwa huu ambao huambukiza chini ya kibofu cha mikojo,huwapata wanaume weusi kwa asili mia kubwa ikilinganishwa na wale wa asili zingine ulimwenguni.

Ili kutambua kuwa mtu anaugua saratani ta tezi kitofu, wataalamu wa afya hufanya  uchunguzi  kwa kutumia kemikali ya “Prostate specific antigen” au PSA katika damu ya mgonjwa, ikiwa kuna idadi ya juu ya PSA , waweza kuwa na ugonjwa huu.

·       Wanaume wengine wamo hatarini kupata saratani ya mamalia dume:

·      Wanaume ambao wamekuwa na jamaa kama baba au kaka ambao   washauguwa ugonjwa huu.

·         Kula vyakula vingi vya mafuta, nyama nyekundu, siagi na maziwa. 

Dalili ya saratani ya mamalia dume:

·          Kukojoakojoa kila mara hasa wakati wa siku.

·          Kuwa na shida za kuanza kukojoa au kusitiri mikojo.

·          Kukojoa kwa matone matone.

·          Kuhisi uchungu au moto unapokojoa

·          Kuhisi uchungu unapomwaga manii.

·          Kukojoa mikojo iliyochanganyika na damu. 

 

Alhamisi, 10 Oktoba 2013


 The 2013 International Conference on Family Planning: 


Family Planning






Katika juhudi za kuboresha afya ya akina mama,shirika la mpango uzazi duniani litafanya Mkutano wa Mpango uzazi  nchini Ethiopia mwezi wa Novemba mwaka huu.










Mkutano huu unafanyika huku karibu watu millioni 900 kote duniani wakikumbatia uzazi wa mpango.

Hata hivyo, sio wote wanaoweza kufanya uzazi wa mpango wakati wanapotaka kufuatia changamoto kadha wa kadha.

Mkutano huu utawajumuisha watafiti wa afya,madaktari na wadau wengine katika sekta ya afya.


Inaaminika kuwa wazazi wengi ambao wangependa kupanga uzazi wanasubuka sana.Hata kabla wapate huduma hiyo muhimu wanagundua kuwa ni wajawazito.Idadi ya wanandoa walio kwenye hali hii ni zaidi ya millioni 215 kote duniani.

 Uzazi wa mpango unawezesha wanandoa kufanya maamuzi ya uzazi na ni moja ya njia ya gharama nafuu kwa ajili ya kuboresha afya  ya familia. 
Kilingana na takwimu za shirika laThe Bill & Melinda Gates  idadi ya 287,000 ya wanawake hufariki kila mwaka katika hali ya ujauzito.
 




Jumanne, 8 Oktoba 2013





 


Mwezi wa Oktober ni mwezi wa kuelimisha umma jinsi ya kupambana na ugonjwa hatari wa saratani hususan ile ya matiti.
Hata hivyo juhudu za kupambana na saratani haziridhishi kutokana na ukosefu wa vifaa vya kugundua na kuutibu.



Baadhi ya wakenya wamelalamika kuwa vifaa duni katika hospitali za umma kunachangia ongezeko la idadi ya wanaofariki kila siku kutokana na saratani.

Pia,Upungufu wa watalaamu wa saratani huku baadhi yao kukikimbilia hospitali za binafsi ambapo wanapata mishahara yakulidhisha.

Hivyo basi ni jukumu la serikali kuhakikisha kuna vifaa vya kisasa.Na kuongeza mishahara kwa watalaamu wa afya.
Kwa sasa,idadi kubwa ya wakenya hutafuta matibabu ya saratani nchini India ambapo ghalama ya matibabu ni nafuu.

Hata hivyo, sio kila mtu au jamaa inaweza kugharamia matibabu ya saratani India.
Ni jukumu ya serikali kuhakikisha kuwa wanachi hawafariki kutokana na ugonjwa huu kwa sababu ya gharama au musongamano wa wangonjwa unaopelekewa na upungufu wa vifaa vya matibabu.

Mikakati muhimu na ya dharura inahitajika ili kupungunga au kukambilaiana nahali hii ya kuhuzunisha.
Ugonjwa huu umekuwa tishio nchini kenya na pia nchi zinachoendelea.
Hata hivyo,kuna sababu ya kutokufaa moyo ,kwani ugonjwa unapogunduliwa mapema,mgonjwa anaweza akapona.

Baadhi ya dalili ni kama vile;
-Kuwepo kwa uvimbe kwenye sehemu za kwapa
-Sehemu ya titi kuingia ndani 
-Mabadiliko kwenye chuchu
-kidonda kwenye chuchu
-chuchu hutokwa damu au maji yasiyo ya kawaida
 -ngozi kuwa na rangi nyekundu.