Jumatano, 16 Oktoba 2013

 

Saratani tezi

Huku ukiwa mwezi wa kupambana na janga la ugonjwa wa saratani,watu wengi hawapendi  kwenda hospitalini kwa uchunguzi,huku wakihofia kugunduliwa na maradhi ya saratani.
Hii ni baadhi ya sababu zinazopelekea ongezeko la saratani nchini kenya na kanda la afrika kwa jumla.
Inakisiwa kuwa zaidi ya watu elfu moja(1,000)  huugua saratani huku zaidi ya  850 wakifariki kila mwaka.
Takwimu pia zinaonyesha idadi ya saratani ya tezi kibofu inaongezeka marudufu.

Saratani ya tezi kibofu ni ugonjwa ambao  huwa kati ya wanaume.kama aina nyingine za saratani, inapogunduliwa mapema inakuwa ni rahisi kutibiwa. Zaidi ya hayo, walio  hatarini ya kuambukizwa Ugonjwa huu ni  wanaume walio na umri wa miaka 55 na zaidi.

 Kulingana na watalaamu wa afya watu wengi hutafuta tiba wakati ugojwa umeenea zaidi.

Hivi majuzi, ugonjwa wa saratani umetia wengi kiwewe.Siku baada ya siku kuna habari kuwa mtu fulani ana ugonjwa wa saratani.Waume kwa wanawake,vijana  kwa watoto wote wako hatarini ya kuabukizwa ugonjwa huu.

Watafiti bado hawajapata uvubuzi ni nini haswa inayo sababisha ugonjwa huu hatari.

Hata hivyo inakisiwa kuwa  mazingira tunayoishi, kwa njia moja ua nyingine yanachangia kuwepo kwa maradhi haya.

Waziri Mwenzake, Prof. Anyang Nyongo pia aligunduliwa kuugua saratani ya tezi kibofu.Kwa bahati nzuri, iligunduliwa mapema na baada ya matibabu ya muda, madaktari walimhakikishia  kuwa amepona.

Pia mwanahabari mashuhuri Jerry Okungu ana saratabni ya tezi kibofu.Amekuwa akikabiriana na ugonjwa huu kwa muda sasa.Afueni ni kuwa haja kata tamaa na ameanzisha wakfu wa saratani ili kuwaelimisha na kuwasaidia wale wasioweza kugharamia matibabu.

 

Matibabu ya saratani huwa ghali mno,hivyo basi wale wanaougua wanakubwa na matatizo ya kutafuta matibabu,hii huchangia kuzorota kwa afya na hata maafa.

Ugonjwa huu ambao huambukiza chini ya kibofu cha mikojo,huwapata wanaume weusi kwa asili mia kubwa ikilinganishwa na wale wa asili zingine ulimwenguni.

Ili kutambua kuwa mtu anaugua saratani ta tezi kitofu, wataalamu wa afya hufanya  uchunguzi  kwa kutumia kemikali ya “Prostate specific antigen” au PSA katika damu ya mgonjwa, ikiwa kuna idadi ya juu ya PSA , waweza kuwa na ugonjwa huu.

·       Wanaume wengine wamo hatarini kupata saratani ya mamalia dume:

·      Wanaume ambao wamekuwa na jamaa kama baba au kaka ambao   washauguwa ugonjwa huu.

·         Kula vyakula vingi vya mafuta, nyama nyekundu, siagi na maziwa. 

Dalili ya saratani ya mamalia dume:

·          Kukojoakojoa kila mara hasa wakati wa siku.

·          Kuwa na shida za kuanza kukojoa au kusitiri mikojo.

·          Kukojoa kwa matone matone.

·          Kuhisi uchungu au moto unapokojoa

·          Kuhisi uchungu unapomwaga manii.

·          Kukojoa mikojo iliyochanganyika na damu. 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni