Jumanne, 8 Oktoba 2013





 


Mwezi wa Oktober ni mwezi wa kuelimisha umma jinsi ya kupambana na ugonjwa hatari wa saratani hususan ile ya matiti.
Hata hivyo juhudu za kupambana na saratani haziridhishi kutokana na ukosefu wa vifaa vya kugundua na kuutibu.



Baadhi ya wakenya wamelalamika kuwa vifaa duni katika hospitali za umma kunachangia ongezeko la idadi ya wanaofariki kila siku kutokana na saratani.

Pia,Upungufu wa watalaamu wa saratani huku baadhi yao kukikimbilia hospitali za binafsi ambapo wanapata mishahara yakulidhisha.

Hivyo basi ni jukumu la serikali kuhakikisha kuna vifaa vya kisasa.Na kuongeza mishahara kwa watalaamu wa afya.
Kwa sasa,idadi kubwa ya wakenya hutafuta matibabu ya saratani nchini India ambapo ghalama ya matibabu ni nafuu.

Hata hivyo, sio kila mtu au jamaa inaweza kugharamia matibabu ya saratani India.
Ni jukumu ya serikali kuhakikisha kuwa wanachi hawafariki kutokana na ugonjwa huu kwa sababu ya gharama au musongamano wa wangonjwa unaopelekewa na upungufu wa vifaa vya matibabu.

Mikakati muhimu na ya dharura inahitajika ili kupungunga au kukambilaiana nahali hii ya kuhuzunisha.
Ugonjwa huu umekuwa tishio nchini kenya na pia nchi zinachoendelea.
Hata hivyo,kuna sababu ya kutokufaa moyo ,kwani ugonjwa unapogunduliwa mapema,mgonjwa anaweza akapona.

Baadhi ya dalili ni kama vile;
-Kuwepo kwa uvimbe kwenye sehemu za kwapa
-Sehemu ya titi kuingia ndani 
-Mabadiliko kwenye chuchu
-kidonda kwenye chuchu
-chuchu hutokwa damu au maji yasiyo ya kawaida
 -ngozi kuwa na rangi nyekundu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni