Huku ugonjwa wa Zika ukiendelea kuenea kwa kasi,kampuni ya dawa ya ufaransa -Sanofi Pasteur iko katika
harakati na shughuli za kukomesha virusi
vya Zika.
Kwa sasa kuna mikakati ya kufanya utafiti wa chanjo kwa binadamu ili
kuepuka adhari za ugonjwa wa Zika.Ingawa utafiti wa chanjo huchukua muda- mrefu,miaka ishirini na zaidi- kundi hili lina matumaini kuwa watafanya wawezalo kuhakikisha tiba imepatikana kwa muda mfupi.
Zaidi ya hayo,Mtafiti Jackson,ananukuliwa akisema ,kampuni ya Sanofi Pasteur inaweza kutumia ufundi,vifaa na uzoefu vilivyotumia katika utafiti na utengenezaji wa chanjo ya virusi ya Dengue miaka kadha iliyopita,katika shughuli za utafiti na chanjo ya virusi vya Zika.
Kampuni hiyo ina umaarufu na pia inaongoza duniani katika utafiti wa chanjoya virusi vya Homa ya Majano.Chanjo yake ilipata kibali cha kutumiwa katika nchi za Brazil,Mexico na ufilipino.
Sanofi imechukua hatua ambayo tayari kampuni zingine za dawa kama vile; Bharat
Biotech ya India, Inovio naTaasisi ya afya ya kitaifa ya Marekani( U.S. National Institutes of Health) -kampuni za
marekani zimezindua utafiti wa tiba ya Zika.
Jaribioya chanjo hiyo kwa
binadamu henda ikawa mwaka ujao,ikiwa mikakati iliowekwa itafikiwa bila shida
yeyote.
Haijabainika hakika ikiwa virusi vya Zika vinasababisha motto kzaliwa na
kichwa kidogo ,lakini kuna uhusiana wa kuabatanisha hali hiyo na virusi hivyo.
Shirika la Afya Duniani(WHO) linakisia kuna idadi ya 15 kampuni na
wasomi ambao kwa sasa wanatafiti tiba ya Zika.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni