Jumatano, 13 Novemba 2019

kongamano laicpd 25



Uhuru Kenyatta welcomes delegates at the Summit's opening. © Nairobi Summit


Rais uhuru Kenyatta afungua rasmi Kongamano la idadi ya watu na maendeleo ICPD25 jiji Nairobi .
Rais amehakikisha kuwa serikali ya Kenya itaweka mikakati ya kuhakikisha kuwa swala la ukeketaji wa wanawake limekabiliwa .

Pia ametaka mataifa menginekuhakikisha haki za wanawake na jamii zinaheshimiwa.
Upashaji tohara nchi na pia barani Afrika imekuwa ikiendelea licha ya hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika.

Kulingana na tafiti wanawake waliopashwa tohara wanakuwa  hatarini wanapojifungua huku wengine wakifariki wakati wa kujifungua.


ICPD 25 NAIROBI



Image result for https://www.nairobisummit demo
Kongamana kuu la kimataifa limengoa nanga  nchini Kenya huku maswala ya afya ya uzazi yakiorodheshwa kuwa kipaombele kati ya maswala nyeti yatakayo jadiliwa.

Isistoshe,malengo makuu tano yanayolengwa katika mjadala wa siku tatu wa kongamano la (ICPD25) ni kama vile ; haki ya afya ya uzazi,dhuluma za kijinsia na tabia tofauti ambazo zinaadhiri wanawake.

Hata hivyo kuna baadhi ya vikundi ambavyo vina tofautiana na mkutano huu, hususan kuhusu maswala  ya uaviaji mimba na ngono za jinsia sawa yaani ushoga na ushagaji.

Mashirika ya kidini yalipinga kuwa endapo maswala haya yatapewa nafasi ya kwanza, hawatahudhuria,huku wakisisitiza kuwa yanapinzana na desturi na mwelekeo wa dini.
Vingozi wa dini wanakashifu hatua ya mkutano huu kwa kusema kuwa uaviaji mimba ni kitendo ambacho ni dhambi na pia ushoga hauna nafasi katika dini .

Kwa mfano kanisa katoliki duniani hawaruhusu matumizi ya aina yeyote ya uzazi mpango hospitali wanazomiliki na zsisitiza ni dhambi.

Mwaka jana kasisi mmoja alikata kufanya maombi ya wafu kwa mama aliyefariki na aliyedaiwa kuavya mimba.

Hata ikiwa  maswala haya yanajitokeza wakati wa mkutano huu,hakika ni kuwa kuna sababu za kiafya ambazo muunguzi anaweza kumshauri mgonjwa kuavya mimba endapo maisha yake yatakuwa kwenye hatari.

Hata hivyo mkutano uliendelea kama kawaida huku kukiwa na lengo la kurai serikali kuchangia kueneza malengo haya kifedha na pia kisiasa.

Takwimu zilizotolewa zinaonyesha kuwa Kenya ni miongoni mwa nchi sita ambazo zinaendelea kushamili katika maswala ya uzazi mpango, huku idadi ya wanaotumia njia za kisasa za uzazi mpango ikiongezeka.

 Ripoti iliyozinduliwa mkabala na mkutano huu inaonyesha kuwa Kenya imepiga hatua kukumbatia matumizi ya kondomu,sindano na vidonge.

Mkutano huu umeadaliwa na shirika la idadi ya watu na serikali za Kenya na Denmark .
Mkutano kama huu ulifanyika Zaidi ya miaka ishirini huko Cairo,Misri ambako azimio la Cairo lililatibiwa.