COVID -19 Kenya
Huku ugonjwa wa Virusi vya Corona –COVID-19 ukiendele kuenea kwa kasi nje ya uchina ,Serikali ya Kenya imelaumiwa kwa kuruhusu kuingia nchini watu 239 warioabiri ndege ya Uchina. Inadaiwa kuwa abiria hao walitakiwa wasikaribiane au wajitenge na watu kwa muda furani kama tahadhari dhidi ya kuambukiza wa Virusi vya Corona . Hata hivyo kuna hofu kuwa huenda kunauwezekano kuwa mmoja au zaidi ya abiria wakawa na virusi hivyo ambavyo huchukua wiki kabla dhariri zake kuibuka. Ugonjwa huu umewauwa maelfu ya watu nchini uchina na pia mataifa mengine nje ya Uchina yameadhirika. Uchina umekuwa kitovu cha virusi, na kufikia sasa watu 81,291wameambukizwa vurisi hivi ulimwenguni kote na kuwauwa 2,770, wengi wao wakiwa katika taifa la Asia. Virusi vya Corona ambao umepewa jina rasmi Covid-19, mara nyingi huenea kutoka kwa mtu mmoja hadi mtu. Serikali kwa upande wake imesema hakuna haja ya kuhofia maambukizi kwani mikakati dhabiti imewekwa kuhakikisha hakuna mtu ataka...