Gavana Wa Jimbo La Nyamira Aaga Dunia
Gavana wa Kauti ya Nyamira John Obiero Nyagarama afariki dunia.Nyagarama
amekuwa akipokea matibabu katika Nairobi hospital iliyoko jijini Nairobi,kwa
takriban mwezi mmoja.
Inasemekana Gavana
Nyagarama alikuwa anaugua ugonjwa wa COVID-19.
Kulinagana na familia
yake,alikuwa na matatizo ya kupumua baada ya mapafu yake kushindwa kufanya
kazi.
Hata hivyo, Nyangarama
amekuwa na matatizo ya kiafya ila familia yake imesita kusema alichokuwa anaungua
.
Zaidi ya hayo,
alisifika kwa kufanya miradi ya maendeleo kwenye kauti ya Nyamira, na pia
kuwahimiza wakaazi umuhimu wa kujizuia kuambukizwa virusi vya Corona.
Pia
, alikuwa
mkulima Hodari has awa zao la chai.Alifanya kazi katika sekta ya kilimo hususan
majani chai na kupanda ngazi kwa kasi hasi akawa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chai nchini kwa
muda mrefu.
Hapo awali alifunza
katika shule mbalimabli baada ya kufuzu kama mwalimu katika Chuo Kikuu cha Nairobi.Hadi
kifo chake alikuwa na umri wa miaka 74.
Mola ailaze roho
yake mahali pema peponi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni