Reuben
Githinji
Ugonjwa wa
COVID-19 umetupokonya mwanadishi aliyebombea Reuben Githinji.
Githinji
aliugua na alihitaji dharula lakini hospitali ya mkoa ya Embu,haikuwa na
nafasi.
Ilibidi
ahamishe hadi Hospitali ya Muranga ambapo alifariki akipokea matibabu.
Nimehuzunishwa
na kifo cha mtu niliye mfahamu kwa muda mrefu na nilimuita kakangu.
Nilikutana naye Reuben Githinhji alipokuwa anandkikia kampuni ya Kenya Times huko Meru.
Nilikuwa
mwandishi wa Habari aliyekuwa anajifunza uanahabari,hivyo basi baadaya ya
rikizo kutoka chuoni tulitakiwa kutafuta nafasi ya miazi nne ili kufijunza nje
ya darasa.
Kwa bahati
nzuri, nilipata nafasi kutoka kwa kampuni ya nation wakanituma, wilaya ya Meru
alipokuwa mwanahabari wao Imanene Imathiu ambaye ni marehemu.
Katika
harakati za kukusanya Habari hapa ana pale nilikutana na Githinji ambaye
alikuwa anapenda sana kazi yake.
Alipenda
sana kuandika kuhusu maswala ya siasa na jamii kwa jumla.
Nkumbuka
wakati ule Kampuni ya Kenya Times ilikuwa inachelewa sana kuwalipa wafanyakazi
wake lakini yeye hakukata tamaa.Alijitolea kufanya kazi kwa moyo wake wote.
Hadi Kenya
Times walipofunga na akajiunga na Kampuni ya Nairobi Star amekuwa mwanahabari
mkakamavu aliyependa kufanya kazi yake bila kusukumwa.
Waliofanya
kazi naye watasema kuwa alipanda milima na mabonde kutafuta Habari na Makala ambayo
ingebadilsha sura ya jamii alimoishi hasa katika majimbo ya Meru na Embu.
Ingawa
tulitumikia kampuni tofauti,tuishi kama familia moja na kusaidiana katika
maswala ya uanahabari.
Mola ailaze
roho yake pema peopni…..
Githinji
lala salama.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni