Ijumaa, 26 Machi 2021

Reuben Githinji

 

Reuben Githinji

Ugonjwa wa COVID-19 umetupokonya mwanadishi aliyebombea Reuben Githinji.

Githinji aliugua na alihitaji dharula lakini hospitali ya mkoa ya Embu,haikuwa na nafasi.

Ilibidi ahamishe hadi Hospitali ya Muranga ambapo alifariki akipokea matibabu.

Nimehuzunishwa na kifo cha mtu niliye mfahamu kwa muda mrefu na nilimuita kakangu.

Nilikutana naye Reuben Githinhji alipokuwa anandkikia kampuni ya Kenya Times huko Meru.

Nilikuwa mwandishi wa Habari aliyekuwa anajifunza uanahabari,hivyo basi baadaya ya rikizo kutoka chuoni tulitakiwa kutafuta nafasi ya miazi nne ili kufijunza nje ya darasa.

Kwa bahati nzuri, nilipata nafasi kutoka kwa kampuni ya nation wakanituma, wilaya ya Meru alipokuwa mwanahabari wao Imanene Imathiu ambaye ni marehemu.

Katika harakati za kukusanya Habari hapa ana pale nilikutana na Githinji ambaye alikuwa anapenda sana kazi yake.

Alipenda sana kuandika kuhusu maswala ya siasa na jamii kwa jumla.

Nkumbuka wakati ule Kampuni ya Kenya Times ilikuwa inachelewa sana kuwalipa wafanyakazi wake lakini yeye hakukata tamaa.Alijitolea kufanya kazi kwa moyo wake wote.

Hadi Kenya Times walipofunga na akajiunga na Kampuni ya Nairobi Star amekuwa mwanahabari mkakamavu aliyependa kufanya kazi yake bila kusukumwa.

Waliofanya kazi naye watasema kuwa alipanda milima na mabonde kutafuta Habari na Makala ambayo ingebadilsha sura ya jamii alimoishi hasa katika majimbo ya Meru na Embu.

Ingawa tulitumikia kampuni tofauti,tuishi kama familia moja na kusaidiana katika maswala ya uanahabari.

Mola ailaze roho yake pema peopni…..

Githinji lala salama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni