endometrial cancer-Saratani ya uterazi

Saratani ya shingo ya  uzazi bado ndiyo aina ya kansa ya uzazi inayoshababisha maafa ya akina mama zaidi nchini Kenya. Takwimu kutoka Kenya Cancer Registry zinaonyesha kwamba zaidi ya wanawake 5,200 hugunduliwa kuwa na saratani ta Uterine  kila mwaka, na hiyo ni karibu asilimia 20 ya wanawake wote wanaopata ugonjwa huo.Inasikitisha kuwa zaidi ya wanawake 3,200 hufa kila mwaka, hii ikiwa sababu  kuu ya idadi kubwa ya vifo vinavyohusiana na saratani miongoni mwa wanawake, ya pili  baada ya kansa ya matiti inayoongaza.


Kulingana na wataalamu wa afya saratani ya shingo ya  uzazi inaweza kuzuiwa kwa uchunguzi wa kawaida na chanjo ya HPV, hii inaweza kupunguza visa vingi vya magonjwa haya, anasema Dk. Gladys Mugambi, afisa mwandamizi wa Wizara ya Afya. Mugambi anasema shughuli ya kutafuta chanjo na wagonjwa  bado ni ya chini sana, hasa katika maeneo ya vijijini.

 kechelewa kutafuta tiba

Mojawapo ya changamoto kubwa za Kenya ni kugunduliwa kwa magonjwa . Uchunguzi unaonyesha kwamba zaidi ya asilimia 90 ya wanawake hupatwa na ugonjwa huo lakini wanatafuta matibabu ya afya  baadaye, wakati ugonjwa umeenea Zaidi.Zaidi ya hayo,  matibabu ni magumu kepata bila pesa kwani  ni ghali.

Tafiti zinaonyasha kuwa ni asilimia 14-18 tu ya wanawake wa Kenya wenye umri wa kati ya miaka 18 na 69 ambao wamewahi kuchunguzwa endapo wanaugua  saratani ya kizazi, hki ni kiwango cha chini sana kilingana na malengo ya WHO la kufikia asilimia 70 ya uchunguzi kufikia mwaka 2030.

Hali ni mbaya sana katika kaunti kama vile Kisumu, ambapo chini ya asilimia 6 ya wanawake  walipimwa mwaka 2019. Mara kwa mara, vituo vya afya havina vifaa vya kugundua ugonjwa huo mapema, na bado wanawake wengi hawaendi kwenye vituo vya uchunguzi kwa sababu ya ubaguzi wa kitamaduni au vituo vya afya viko mbali na makao yao.

picha ya Cleveland Clinic
 Saratani  tofauti za uzazi zinaongezeka

 Ingawa saratani ya  uzazi ndiyo inayoongoza, saratani  nyingine za mfumo wa uzazi zinaongezeka pia:

Kansa ya ovari: takwimu zinaonyesha kuwa kuna visa nyingi ulimwenguni.Karibu visa vipya vilivyo ripotiwa ni kama vile; 90,000 mnamo 2022, na zaidi ya vifo 32,000. Nchini Kenya, kiwango cha kuudhibiti chaendelea kuwa cha chini kwa sababu ya ukosefu wa matibabu maalum. Saratani ya kizazi (endometrial), Ilirekodiwa visa vipya 60,000 ulimwenguni kote mnamo 2022, lakini eimu au uhamazisho kuhusu saratani hii ni mchache  nchini Kenya .

 Saratani za uzazi za kiume hasa saratani ya kibofu cha mkojo sasa ni moja ya kansa za kawaida miongoni mwa wanaume wa Kenya, pamoja na saratani ya testicular, ambayo ingawa ni nadra, huathiri  hasa wanaume wa umri mdogo.

Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) linasema kwamba zaidi ya asilimia 90 ya vifo vinavyotokana na saratani ya kibofu hutokea katika nchi zenye mapato ya chini na ya kati. Chanjo ya HPV, ambayo sasa inapatikana nchini Kenya kwa wasichana wenye umri wa miaka 10-14 ina uwezo wa kupunguza kwa kiasi kikubwa maambukizi mapya iwapo kiwango cha maambukizi kitaongezeka.

Hata hivyo, maendeleo hayafanyiwi kwa usawa. Katika maeneo fulani ya mashambani, habari za kupotosha ,tamaduni na mila  kuhusu chanjo zimedhoofisha kampeni za chanjo. Wakati huohuo, miundombinu ya uchunguzi na matibabu ingali imejikita katika vituo vya mijini kama Nairobi na Mombasa, na kuwaacha wanawake katika maeneo ya mbali kuwa hatarini.

Mikakati ya kudhibiti saratani

Kenya imepitisha mkakati wa Kimataifa wa WHO wa kuukabili ugonjwa wa Saratani ya Shingo ya Uzazi, ambao unaweka malengo makubwa kama vile;

·         Asilimia 90 ya wasichana wamechanjwa kabisa dhidi ya HPV kufikia umri wa miaka 15

·         Asilimia 70 ya wanawake kuchunguzwa angalau mara mbili katika maisha yao

·         Asilimia 90 ya wanawake walio na ugonjwa wa kabla ya kansa au kansa wanaopokea matibabu

Kutimiza malengo haya itahitaji uwekezaji mkubwa, kampeni za uhamasishaji, na kuvunja ukimya kuzunguka afya ya uzazi.

"Ugonjwa wa saratani ya kizazi si suala la matibabu tu, ni suala la haki ya kijamii", anasema Dkt. Esther Mwaura, mtetezi wa afya ya uzazi.  Anasema hakuna mwanamke anayepaswa kufa kutokana na ugonjwa ambao tayari tunajua jinsi ya kuuzuia.

Hatua muhimu

Kadiri visa vya saratani vinavyoongezeka, wataalamu wanaonya kwamba kunyamaza na unyanyapaa kunaweza kusababisha kifo. Kutoa elimu and kuendelea na  chanjo ya HPV, kuongeza mipango ya uchunguzi, na kuimarisha vituo vya huduma ya saratani ndiyo njia muhimu ambayo Kenya inaweza kukabiliana na hali hiyo.

Kwa sasa  maelfu ya wanawake na wanaume, wako kwenye hatari endapo hatua za dharula za kuudhibiti ugonjwa huu hazitachukuliwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Global Health Leaders Rally in Bogotá to Tackle Reproductive Health Gaps

Unsafe Abortion